< Hosea 13 >
1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
When Ephraim spake, there was trembling; he exalted himself in Israel: but when he offended in Baal, he died.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
And now they sin more and more, and have made them molten images of their silver, even idols according to their own understanding, all of them the work of the craftsmen: they say of them, Let the men that sacrifice kiss the calves.
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
Therefore they shall be as the morning cloud, and as the dew that passeth early away, as the chaff that is driven with the whirlwind out of the threshing-floor, and as the smoke out of the chimney.
4 “Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
Yet I am the LORD thy God from the land of Egypt; and thou shalt know no god but me, and beside me there is no saviour.
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
I did know thee in the wilderness, in the land of great drought.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
According to their pasture, so were they filled; they were filled, and their heart was exalted: therefore have they forgotten me.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
Therefore am I unto them as a lion: as a leopard will I watch by the way:
8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
I will meet them as a bear that is bereaved of her whelps, and will rend the caul of their heart: and there will I devour them like a lion; the wild beast shall tear them.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
It is thy destruction, O Israel, that [thou art] against me, against thy help.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
Where now is thy king, that he may save thee in all thy cities? and thy judges, of whom thou saidst, Give me a king and princes?
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
I have given thee a king in mine anger, and have taken him away in my wrath.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
The iniquity of Ephraim is bound up; his sin is laid up in store.
13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
The sorrows of a travailing woman shall come upon him: he is an unwise son; for it is time he should not tarry in the place of the breaking forth of children.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol )
I will ransom them from the power of the grave; I will redeem them from death: O death, where are thy plagues? O grave, where is thy destruction? repentance shall be hid from mine eyes. (Sheol )
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
Though he be fruitful among his brethren, an east wind shall come, the breath of the LORD coming up from the wilderness, and his spring shall become dry, and his fountain shall be dried up: he shall spoil the treasure of all pleasant vessels.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
Samaria shall bear her guilt; for she hath rebelled against her God: they shall fall by the sword; their infants shall be dashed in pieces, and their women with child shall be ripped up.