< Hosea 13 >

1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
When Ephraim spoke, there was trembling, he exalted himself in Israel; but when he became guilty through Baal, he died.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
And now they sin more and more, and have made them molten images of their silver, according to their own understanding, even idols, all of them the work of the craftsmen; of them they say: 'They that sacrifice men kiss calves.'
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
Therefore they shall be as the morning cloud, and as the dew that early passeth away, as the chaff that is driven with the wind out of the threshing-floor, and as the smoke out of the window.
4 “Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
Yet I am the LORD thy God from the land of Egypt; and thou knowest no God but Me, and beside Me there is no saviour.
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
I did know thee in the wilderness, in the land of great drought.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
When they were fed, they became full, they were filled, and their heart was exalted; therefore have they forgotten Me.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
Therefore am I become unto them as a lion; as a leopard will I watch by the way;
8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
I will meet them as a bear that is bereaved of her whelps, and will rend the enclosure of their heart; and there will I devour them like a lioness; the wild beast shall tear them.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
It is thy destruction, O Israel, that thou art against Me, against thy help.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
Ho, now, thy king, that he may save thee in all thy cities! and thy judges, of whom thou saidst: 'Give me a king and princes!'
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
I give thee a king in Mine anger, and take him away in My wrath.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
The iniquity of Ephraim is bound up; his sin is laid up in store.
13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
The throes of a travailing woman shall come upon him; he is an unwise son; for it is time he should not tarry in the place of the breaking forth of children.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol h7585)
Shall I ransom them from the power of the nether-world? Shall I redeem them from death? Ho, thy plagues, O death! Ho, thy destruction, O nether-world! Repentance be hid from Mine eyes! (Sheol h7585)
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
For though he be fruitful among the reed-plants, an east wind shall come, the wind of the LORD coming up from the wilderness, and his spring shall become dry, and his fountain shall be dried up; he shall spoil the treasure of all precious vessels.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
Samaria shall bear her guilt, for she hath rebelled against her God; they shall fall by the sword; their infants shall be dashed in pieces, and their women with child shall be ripped up.

< Hosea 13 >