< Hosea 13 >
1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
While Ephraim was speaking, a horror entered Israel, and he offended by Baal, and he died.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
And now they add that they will be sinning more. And they have made themselves an image cast from their silver, just like the image of idols; but the whole thing has been made by craftsmen. These say to them, “Sacrifice men, you who adore calves.”
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
For this reason, they will be like the morning clouds, and like the morning dew that passes away, just like the dust that is driven by a whirlwind away from the threshing floor, and like the smoke from a chimney.
4 “Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
But I am the Lord your God from the land of Egypt, and you will not know God apart from me, and there is no Savior except me.
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
I knew you in the desert, in the land of solitude.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
According to their pastures, they have been filled up and have been satisfied. And they have lifted up their heart, and they have forgotten me.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
And I will be to them like a lioness, like a leopard in the way of the Assyrians.
8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
I will run to meet them like a bear that has been robbed of her young, and I will split open the middle of their liver. And I will devour them there like a lion; the beast of the field will tear them apart.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
Perdition is yours, Israel. Your help is only in me.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
Where is your king? Now, especially, let him save you in all your cities, and from your judges, about whom you said, “Give me kings and princes.”
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
I will give you a king in my wrath, and I will take him away in my indignation.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
The iniquity of Ephraim has been bound; his sin has been engulfed.
13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
The pains of giving birth will reach him. He is an unwise son. For now he will not remain firm during the contrition of his sons.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol )
I will free them from the hand of death; from death I will redeem them. Death, I will be your death. Hell, I will be your deadly wound. Consolation is hidden from my eyes. (Sheol )
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
For he will make a division among brothers. The Lord will bring a burning wind, rising up from the desert, and it will dry up his streams, and it will make his fountain desolate, and he will tear apart every collection of desirable useful things.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
Let Samaria perish, because she has urged her God towards bitterness. Let them perish by the sword, let their little ones be thrown down, and let their pregnant women be cut in two.