< Hosea 13 >
1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
Když mluvíval Efraim, býval strach; vznešený byl v Izraeli, ale prohřešiv při Bálovi, tožť umřel.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
A i nyní ještě předce hřeší. Nebo dělají sobě a slévají z stříbra svého podlé rozumu svého strašidla, ješto všecko to není než dílo řemeslníků, o čemž říkají: Lidé, kteříž obětují, telata ať líbají.
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
Protož budou jako oblak ranní a jako rosa jitřní, kteráž odchází, jako plevy vichřicí zachvácené z humna, a jako dým z komínu,
4 “Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
Ješto já jsem Hospodin Bůh tvůj od vyjití z země Egyptské, a Boha kromě mne nepoznal jsi, aniž jest jiný vysvoboditel kromě mne.
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
Jáť jsem tě poznal na poušti v zemi velmi vyprahlé.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
Dobré pastvy měvše, nasyceni jsou, ale když se nasytili, pozdvihlo se srdce jejich, protož zapomenuli na mne.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
Pročež budu jim jako lítý lev, jako pardus vedlé cesty číhati budu.
8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
Potkám se s nimi jako nedvěd osiřelý, a roztrhám všecko srdce jejich, a sežeru je tam jako lev, jako zvěř divoká roztrhující je.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
Z tebeť jest zhouba tvá, ó Izraeli, ješto ve mně všecka pomoc tvá.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
Kdež jest král tvůj? Kdež jest? Nechť tě zachová ve všech městech tvých. Aneb soudcové tvoji, o nichž jsi řekl: Dej mi krále a knížata?
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
Dal jsem tobě krále v hněvě svém, a odjal jsem v prchlivosti své.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
Svázánať jest nepravost Efraimova, schován jest hřích jeho.
13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
Bolesti rodičky přijdou na něj; jest syn nemoudrý, sic jinak nezůstával by tak dlouho v životě matky.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol )
Z ruky hrobu vyplatím je, od smrti vykoupím je; budu zhoubcím tvým, ó smrti, budu zkažením tvým, ó hrobe, želení skryto bude od očí mých. (Sheol )
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
Nebo on mezi bratřími ovoce ponese, ač prv přijde vítr východní, vítr Hospodinův od pouště vstupující, a vysuší studnice jeho, osuší i vrchoviště jeho; onenno rozchvátá poklad všech nejdražších klénotů.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
Zpuštěna bude Samaří, proto že se protivila Bohu svému; od meče padnou, dítky jejich zrozrážíny budou, a těhotné ženy jejich zroztínány.