< Hosea 10 >

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
Israel er et frodig vintre, som bærer frukt; jo mere frukt han fikk, desto flere alter bygget han; jo bedre det gikk hans land, desto vakrere billedstøtter gjorde han sig.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
Deres hjerte er falskt, nu skal de bøte; han skal bryte ned deres altere og ødelegge deres billedstøtter;
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
ja, nu skal de si: Vi har ingen konge; for vi har ikke fryktet Herren, og kongen, hvad kan vel han gjøre for oss?
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
De har talt tomme ord, svoret falsk, inngått forbund, og retten skyter op som giftige urter på markens furer.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
For Bet-Avens kalv er Samarias innbyggere i angst; ja, dens folk sørger over den, og dens avgudsprester skjelver for den - for dens herlighet, fordi den er ført bort fra dem.
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
Også den skal føres til Assur, som en gave til kong Jareb; skam skal Efra'im høste, og Israel skal skamme sig over sitt råd.
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
Samarias konge skal bli borte som en spån på vannets flate.
8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
Og Avens offerhauger, Israels synd, skal tilintetgjøres; torner og tistler skal skyte op på deres altere, og de skal si til fjellene: Skjul oss! og til haugene: Fall over oss!
9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
Fra Gibeas dager av har du syndet, Israel! Der er de blitt stående, uten at krigen mot nidingene har nådd dem i Gibea.
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
Efter min lyst vil jeg tukte dem, og folkeslag skal samles imot dem, når jeg binder dem fast til begge deres misgjerninger.
11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
Efra'im er en opøvd kvige, som gjerne vil treske, men jeg legger et åk på dens fagre hals; jeg vil spenne Efra'im for, Juda skal pløie, Jakob skal harve.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
Så eder en sæd, som rettferdigheten krever, få eder en høst efter kjærlighetens bud, bryt eder nytt land! For nu er det tiden til å søke Herren, til han kommer og lar rettferdighet regne over eder.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
I har pløid ugudelighet, I har høstet urett, I har ett løgnens frukt; for du har satt din lit til din ferd og til dine mange helter.
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
Derfor skal det reise sig et krigsbulder blandt dine stammer, og alle dine festninger skal ødelegges, likesom Salman ødela Bet-Arbel på stridens dag, da både mor og barn blev knust.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
Sådant skal Betel føre over eder for eders store ondskaps skyld; når det lysner til dag, er det ute, aldeles ute med Israels konge.

< Hosea 10 >