< Hosea 10 >

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
Israël est une vigne luxuriante qui produit son fruit. Selon l'abondance de ses fruits, il a multiplié ses autels. Au fur et à mesure que leurs terres ont prospéré, ils ont orné leurs pierres sacrées.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
Leur cœur est divisé. Maintenant, ils seront reconnus coupables. Il démolira leurs autels. Il détruira leurs pierres sacrées.
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
Maintenant, ils diront: « Nous n'avons pas de roi, car nous ne craignons pas Yahvé; et le roi, que peut-il faire pour nous? »
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
Ils font des promesses, jurent faussement en concluant des pactes. C'est pourquoi le jugement pousse comme de l'herbe empoisonnée dans les sillons du champ.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
Les habitants de Samarie seront dans la terreur à cause des veaux de Beth Aven, car son peuple se lamentera sur elle, ainsi que ses prêtres qui s'en sont réjouis, pour sa gloire, car il s'en est éloigné.
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
Elle sera aussi transportée en Assyrie pour être offerte à un grand roi. Ephraïm recevra la honte, et Israël aura honte de son propre conseil.
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
Samarie et son roi s'envolent comme une brindille sur l'eau.
8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
Les hauts lieux de l'Aven, le péché d'Israël, seront détruits. L'épine et le chardon monteront sur leurs autels. Ils diront aux montagnes: « Couvrez-nous! » et aux collines: « Tombez sur nous! »
9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
« Israël, tu as péché depuis le temps de Guibea. Ils sont restés là. La bataille contre les enfants de l'iniquité ne les atteint pas à Gibéa.
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
Quand je le voudrai, je les châtierai; et les nations s'assembleront contre eux quand ils sont liés à leurs deux transgressions.
11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
Ephraïm est une génisse dressée qui aime battre, alors je mettrai un joug sur son beau cou. Je mettrai un cavalier sur Ephraïm. Juda va labourer. Jacob va briser ses mottes.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
Semez pour vous-mêmes dans la justice, récolter selon la bonté. Défrichez votre terrain en friche, car il est temps de chercher Yahvé, jusqu'à ce qu'il vienne et fasse pleuvoir la justice sur vous.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
Vous avez labouré la méchanceté. Vous avez récolté l'iniquité. Vous avez mangé le fruit du mensonge, car tu as eu confiance dans ta voie, dans la multitude de tes guerriers.
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
C'est pourquoi un cri de guerre s'élèvera parmi ton peuple, et toutes vos forteresses seront détruites, comme Shalman a détruit Beth Arbel au jour de la bataille. La mère a été mise en pièces avec ses enfants.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
C'est ainsi que Béthel te traitera, à cause de ta grande méchanceté. Au lever du jour, le roi d'Israël sera détruit.

< Hosea 10 >