< Hosea 10 >
1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
[was] a vine Luxuriant Israel fruit he made for himself when [it] became numerous to fruit his he multiplied the altars according to [the] good of land his they made good sacred pillars.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
It is slippery heart their now they will be held guilty he he will break altars their he will destroy sacred pillars their.
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
For now they will say not a king [belongs] to us for not we fear Yahweh and the king what? will he do for us.
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
They have spoken words they have sworn an oath falsehood they have made a covenant and it sprouts up like poisonous plant justice on [the] furrows of a field.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
For [the] heifers of Beth Aven they will be afraid [the] inhabitant[s] of Samaria for it will mourn on it people its and pagan priests its on it they will tremble on glory its for it has gone into exile from it.
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
Also it to Assyria it will be carried tribute to king Jareb shame Ephraim it will seize and it may be ashamed Israel from own counsel its.
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
[will] be destroyed Samaria king its like a twig on [the] surface of [the] waters.
8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
And they will be destroyed [the] high places of wickedness [the] sin of Israel thorn[s] and thistle[s] it will grow up over altars their and they will say to the mountains cover us and to the hills fall on us.
9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
Since [the] days of Gibeah you have sinned O Israel there they have remained not will it overtake? them in Gibeah war on sons of injustice.
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
At desire my and I will discipline them and they will be gathered on them peoples when harness them to [the] two (iniquities their. *Q(K)*)
11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
And Ephraim [was] a heifer trained [which] loved to thresh and I I passed over [the] goodness of neck its I will cause to draw Ephraim it will plow Judah it will harrow itself Jacob.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
Sow yourselves righteousness reap a mouth of loyalty plow yourselves unplowed ground and [it is] time to seek Yahweh until he will come and he may rain down righteousness for you.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
You have plowed wickedness injustice you have reaped you have eaten [the] fruit of lying for you have trusted in own way your in [the] multitude of warriors your.
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
And it will arise an uproar among people your and all fortresses your it will be devastated like [the] devastation of Shalman Beth Arbel on [the] day of battle mother with children she was dashed in pieces.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
Thus someone will do to you O Beth-el because of [the] evil of wickedness your at dawn certainly he will be destroyed [the] king of Israel.