< Hosea 10 >

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
Israel is a luxuriant vine, That bringeth forth fruit; But according to the abundance of his fruit hath he abounded in altars; According to the goodness of his land hath he made goodly images.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
Their heart is divided; now shall they suffer for it; He will break down their altars, And destroy their images.
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
For soon shall they say, We have no king, Because we fear not Jehovah; What can a king do for us?
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
They utter empty words, Swearing falsely, making covenants, And now judgment springeth up, as hemlock in the furrows of the field.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
For the calf of Bethaven shall the inhabitants of Samaria be in fear; Yea, its people shall grieve for it, And its priests shall tremble for it, Because its glory has departed from it.
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
It shall be carried to Assyria, As a present to the hostile king. Ephraim shall be covered with confusion, And Israel shall be ashamed of his doings,
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
Samaria shall be brought to destruction; Her king shall be as a twig upon the waters.
8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
The high places of Aven, the sin of Israel, shall be destroyed; The thorn and the thistle shall come up on their altars. And they shall say to the mountains, Cover us! And to the hills, Fall on us!
9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
More than in the days of Gibeah hast thou sinned, O Israel! There they stood; The battle in Gibeah against the sons of iniquity did not overtake them.
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
Now will I chastise them according to my pleasure, And the nations shall be gathered together against them, When I shall bind them for their two iniquities.
11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
Ephraim is a trained heifer, that loveth to tread out the corn; But I will lay the yoke upon her fair neck; I will cause Ephraim to draw, Judah shall plough, Jacob shall harrow.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
Sow for yourselves to righteousness, and ye shall reap according to your piety; Break up your fallow ground; For it is a time to seek Jehovah, Till he come and rain righteousness upon you.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
Ye plough wickedness, ye shall reap injustice; Ye shall eat the fruit of falsehood. Because thou trustest in thy way, in the multitude of thy mighty men,
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
There shall arise a tumult among thy people, And all thy fortresses shall be destroyed, As Shalman destroyed Betharbel in the day of battle, When the mother was dashed in pieces with her children.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
Such things shall Bethel bring upon you Because of your great wickedness. In the morning shall the king of Israel be destroyed.

< Hosea 10 >