< Hosea 10 >

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
“Israel [is] an empty vine, He makes fruit like to himself, According to the abundance of his fruit, He has multiplied for the altars, According to the goodness of his land, They have made good standing-pillars.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
Their heart has been divided, now they are guilty, He breaks down their altars, He destroys their standing-pillars.
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
For now they say: We have no king, Because we have not feared YHWH, And the king—what does he do for us?
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
They have spoken words, To swear falsehood in making a covenant, And flourished as a poisonous herb has judgment, on the furrows of a field.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
For the inhabitants of Samaria fear the calves of Beth-Aven, Surely its people have mourned on account of it, And its priests leap about on account of it, Because of its glory, for it has removed from it,
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
Also, it is carried to Asshur, a present to a warlike king, Ephraim receives shame, And Israel is ashamed of its own counsel.
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
Samaria is cut off! Its king [is] as wrath on the face of the waters.
8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
And high places of Aven have been destroyed, the sin of Israel. Thorn and bramble go up on their altars, And they have said to hills, Cover us, And to heights, Fall on us.
9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
From the days of Gibeah you have sinned, O Israel, There they have stood, Battle does not overtake them in Gibeah, Because of sons of perverseness.
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
When I desire, then I bind them, And peoples have gathered against them, When they bind themselves to their two iniquities.
11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
And Ephraim [is] a trained heifer—loving to thresh, And I have passed over on the goodness of its neck, I cause [one] to ride Ephraim, Judah plows, Jacob harrows for him.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
Sow for yourselves in righteousness, Reap according to loving-kindness, Till for yourselves tillage of knowledge, To seek YHWH, Until He comes and shows righteousness to you.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
You have plowed wickedness, Perversity you have reaped, You have eaten the fruit of lying, For you have trusted in your way, In the abundance of your might.
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
And a tumult rises among your people, And all your fortresses are spoiled, As the spoiling of Shalman of Beth-Arbel, In a day of battle, Mother against sons dashed in pieces.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
Thus has Beth-El done to you, Because of the evil of your wickedness, In the dawn a king of Israel is utterly cut off!”

< Hosea 10 >