< Wahebrania 1 >
1 Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
God, who in ancient times, spoke often, and in various ways, to the fathers, by the prophets,
2 lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn )
has, in these last days, spoken to us by a Son, whom he has constituted Lord of all things, by whom, also, he made the universe: (aiōn )
3 Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
who, being in effulgence of his glory, and an exact representation of his character, and controlling all things by his own powerful word, after he had, by himself, made expiation for our sins, sat down at the right hand of the Majesty on high;
4 Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
being exalted as far above the angels, as the name he has inherited, is more excellent than theirs.
5 Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
For, to which of the angels did he at any time say, "Thou art my Son: to-day I have begotten thee"? and again, "I will be his Father, and he shall be my Son"?
6 Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
But when he brings again the First-born into the world, he says, "Let all the angels of God worship him."
7 Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
Whereas, concerning angels, he says, "Who makes winds his angels, and flaming fire his ministers."
8 Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn )
But to the Son, "Thy throne, O God, endures for ever. The scepter of thy kingdom is a scepter of rectitude. (aiōn )
9 Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
Thou hast loved righteousness, and hated iniquity; therefore, God, thy God, has anointed thee with the oil of gladness, above thy associates."
10 Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
And, "Thou, Lord, in the beginning didst lay the foundations of the earth, and the heavens are the works of thy hands.
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
They shall perish, but thou dost remain; and they, as a garment, shall grow old;
12 Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
and, as a vesture, thou wilt fold them up, and they shall be changed: but thou art the same; and they shall be changed; but thou art the same; and thy years shall never fail."
13 Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
Moreover, to which of the angels did he say, at any time, "Sit thou at my right hand, till I make thy enemies thy footstool."
14 Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?
"Are they not all ministering spirits, sent forth to minister for them who shall inherit salvation?"