< Wahebrania 1 >
1 Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
很久以前,上帝曾多次通过不同的方式借由先知向我们的祖先说话;
2 lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn )
在这最后的岁月中,上帝又通过他的儿子向我们说话。上帝指认他继承万物,借由他创造宇宙。 (aiōn )
3 Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
他是上帝的荣耀之光,是上帝性格的显化表现,用其强大的号令支撑万物;当他完成清洁罪恶之事,就会坐在天堂至尊者的右边。
4 Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
他的名比天使更尊贵,所以地位高于天使。
5 Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
照样,基督也没有因成为大祭司而为荣。是哪——上帝曾对他说“你是我的儿子。今天我已成为你的父亲。”
6 Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
上帝派其长子来到这世上,又说:“让上帝所有的天使都膜拜他。”
7 Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
关于天使,他说:“上帝以他的天使为风,以他的仆役为火焰。”
8 Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn )
但是说到他的儿子,他说:“上帝啊!你的宝座必将永恒存在,你王国的权杖是公平的权杖。 (aiōn )
9 Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
你喜爱正义良善,憎恨不法。所以上帝,也就是你的上帝,会为你涂抹欢喜的油膏,以此让你高于其他人。”
10 Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
“主啊!你最初铺设了大地的根基,天也是你双手的作品。
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
它们都会终结,你却会长存;它们会像衣服一样逐渐破旧,
12 Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
你却会把它们像外套一样卷起来。天地就像衣服一样会被更换;只有你永不改变,你的生命也没有穷尽。”
13 Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
上帝可曾向哪个天使说:“你坐在我的右边,等我将你的仇敌放在你的脚下”?
14 Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?
天使呢?天使都是仆从,被派出去为那些将要获得救赎的人效劳。