< Wahebrania 9 >
1 Basi agano lile la kwanza lilikuwa na kanuni zake za kuabudu na pia patakatifu pake pa kidunia.
sa prathamo niyama ārādhanāyā vividharītibhiraihikapavitrasthānena ca viśiṣṭa āsīt|
2 Hema ilitengenezwa. Katika sehemu yake ya kwanza kulikuwa na kinara cha taa, meza na mikate iliyowekwa wakfu; hii sehemu iliitwa Mahali Patakatifu.
yato dūṣyamekaṁ niramīyata tasya prathamakoṣṭhasya nāma pavitrasthānamityāsīt tatra dīpavṛkṣo bhojanāsanaṁ darśanīyapūpānāṁ śreṇī cāsīt|
3 Nyuma ya pazia la pili, palikuwa na sehemu iliyoitwa Patakatifu pa Patakatifu,
tatpaścād dvitīyāyāstiraṣkariṇyā abhyantare 'tipavitrasthānamitināmakaṁ koṣṭhamāsīt,
4 ambapo palikuwa na yale madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba, na lile Sanduku la Agano lililofunikwa kwa dhahabu. Sanduku hili lilikuwa na gudulia la dhahabu lenye mana, ile fimbo ya Aroni iliyochipuka, na vile vibao vya mawe vya Agano.
tatra ca suvarṇamayo dhūpādhāraḥ paritaḥ suvarṇamaṇḍitā niyamamañjūṣā cāsīt tanmadhye mānnāyāḥ suvarṇaghaṭo hāroṇasya mañjaritadaṇḍastakṣitau niyamaprastarau,
5 Juu ya lile Sanduku kulikuwa na makerubi ya Utukufu yakitilia kivuli kile kifuniko ambacho ndicho kiti cha rehema. Lakini hatuwezi kueleza vitu hivi kwa undani sasa.
tadupari ca karuṇāsane chāyākāriṇau tejomayau kirūbāvāstām, eteṣāṁ viśeṣavṛttāntakathanāya nāyaṁ samayaḥ|
6 Basi vitu hivi vilipokuwa vimepangwa, makuhani waliingia daima katika sehemu ya kwanza ya hema ili kufanya taratibu zao za ibada.
eteṣvīdṛk nirmmiteṣu yājakā īśvarasevām anutiṣṭhanato dūṣyasya prathamakoṣṭhaṁ nityaṁ praviśanti|
7 Lakini ni kuhani mkuu peke yake aliyeingia ndani ya sehemu ya pili ya hema. Tena hii ilikuwa mara moja tu kwa mwaka, na hakuingia kamwe bila damu, ambayo alitoa kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi za watu walizotenda bila kukusudia.
kintu dvitīyaṁ koṣṭhaṁ prativarṣam ekakṛtva ekākinā mahāyājakena praviśyate kintvātmanimittaṁ lokānām ajñānakṛtapāpānāñca nimittam utsarjjanīyaṁ rudhiram anādāya tena na praviśyate|
8 Kwa njia hii, Roho Mtakatifu alikuwa anaonyesha kwamba, maadamu ile hema ya kwanza ilikuwa bado imesimama, njia ya kuingia Patakatifu pa Patakafifu ilikuwa bado haijafunguliwa.
ityanena pavitra ātmā yat jñāpayati tadidaṁ tat prathamaṁ dūṣyaṁ yāvat tiṣṭhati tāvat mahāpavitrasthānagāmī panthā aprakāśitastiṣṭhati|
9 Huu ulikuwa mfano kwa ajili ya wakati wa sasa, kuonyesha kwamba sadaka na dhabihu zilizokuwa zikitolewa hazikuweza kusafisha dhamiri ya mtu anayeabudu.
tacca dūṣyaṁ varttamānasamayasya dṛṣṭāntaḥ, yato hetoḥ sāmprataṁ saṁśodhanakālaṁ yāvad yannirūpitaṁ tadanusārāt sevākāriṇo mānasikasiddhikaraṇe'samarthābhiḥ
10 Lakini hizi zilishughulika tu na vyakula na vinywaji, pamoja na taratibu mbalimbali za kunawa kwa nje, kanuni kwa ajili ya mwili zilizowekwa hadi wakati utimie wa matengenezo mapya.
kevalaṁ khādyapeyeṣu vividhamajjaneṣu ca śārīrikarītibhi ryuktāni naivedyāni balidānāni ca bhavanti|
11 Kristo alipokuja akiwa Kuhani Mkuu wa mambo mema ambayo tayari yameshawasili, alipitia kwenye hema iliyo kuu zaidi na bora zaidi, ambayo haikutengenezwa kwa mikono ya binadamu, hii ni kusema, ambayo si sehemu ya uumbaji huu.
aparaṁ bhāvimaṅgalānāṁ mahāyājakaḥ khrīṣṭa upasthāyāhastanirmmitenārthata etatsṛṣṭe rbahirbhūtena śreṣṭhena siddhena ca dūṣyeṇa gatvā
12 Hakuingia kwa njia ya damu ya mbuzi na ya ndama; lakini aliingia Patakatifu pa Patakatifu mara moja tu kwa damu yake mwenyewe, akiisha kupata ukombozi wa milele. (aiōnios )
chāgānāṁ govatsānāṁ vā rudhiram anādāya svīyarudhiram ādāyaikakṛtva eva mahāpavitrasthānaṁ praviśyānantakālikāṁ muktiṁ prāptavān| (aiōnios )
13 Damu ya mbuzi na ya mafahali, na majivu ya mitamba walivyonyunyiziwa wale waliokuwa najisi kwa taratibu za kiibada viliwatakasa, hata kuwaondolea uchafu wa nje.
vṛṣachāgānāṁ rudhireṇa gavībhasmanaḥ prakṣepeṇa ca yadyaśucilokāḥ śārīriśucitvāya pūyante,
14 Basi ni zaidi aje damu ya Kristo, ambaye kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na waa, itatusafisha dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo mauti, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai! (aiōnios )
tarhi kiṁ manyadhve yaḥ sadātanenātmanā niṣkalaṅkabalimiva svameveśvarāya dattavān, tasya khrīṣṭasya rudhireṇa yuṣmākaṁ manāṁsyamareśvarasya sevāyai kiṁ mṛtyujanakebhyaḥ karmmabhyo na pavitrīkāriṣyante? (aiōnios )
15 Kwa sababu hii Kristo ni mpatanishi wa agano jipya, ili kwamba wale walioitwa waweze kupokea ile ahadi ya urithi wa milele: kwa vile yeye alikufa awe ukombozi wao kutoka kwa dhambi walizozitenda chini ya agano la kwanza. (aiōnios )
sa nūtananiyamasya madhyastho'bhavat tasyābhiprāyo'yaṁ yat prathamaniyamalaṅghanarūpapāpebhyo mṛtyunā muktau jātāyām āhūtalokā anantakālīyasampadaḥ pratijñāphalaṁ labheran| (aiōnios )
16 Kwa habari ya wosia, ni muhimu kuthibitisha kifo cha yule aliyeutoa,
yatra niyamo bhavati tatra niyamasādhakasya bale rmṛtyunā bhavitavyaṁ|
17 kwa sababu wosia huwa na nguvu tu wakati mtu ameshakufa; kamwe hauwezi kutumika wakati yule aliyeuandika bado yuko hai.
yato hatena balinā niyamaḥ sthirībhavati kintu niyamasādhako bali ryāvat jīvati tāvat niyamo nirarthakastiṣṭhati|
18 Hii ndiyo sababu hata lile agano la kwanza halikuweza kutekelezwa pasipo damu.
tasmāt sa pūrvvaniyamo'pi rudhirapātaṁ vinā na sādhitaḥ|
19 Mose alipotangaza kila amri kwa watu wote, alichukua damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji, sufu nyekundu na matawi ya mti wa hisopo, akanyunyizia kile kitabu na watu wote.
phalataḥ sarvvalokān prati vyavasthānusāreṇa sarvvā ājñāḥ kathayitvā mūsā jalena sindūravarṇalomnā eṣovatṛṇena ca sārddhaṁ govatsānāṁ chāgānāñca rudhiraṁ gṛhītvā granthe sarvvalokeṣu ca prakṣipya babhāṣe,
20 Alisema, “Hii ndiyo damu ya agano, ambalo Mungu amewaamuru kulitii.”
yuṣmān adhīśvaro yaṁ niyamaṁ nirūpitavān tasya rudhirametat|
21 Vivyo hivyo alinyunyizia damu hiyo kwenye ile hema pamoja na kila kifaa kilichotumika ndani yake kwa taratibu za ibada.
tadvat sa dūṣye'pi sevārthakeṣu sarvvapātreṣu ca rudhiraṁ prakṣiptavān|
22 Kwa kweli sheria hudai kwamba, karibu kila kitu kitakaswe kwa damu, wala pasipo kumwaga damu, hakuna msamaha wa dhambi.
aparaṁ vyavasthānusāreṇa prāyaśaḥ sarvvāṇi rudhireṇa pariṣkriyante rudhirapātaṁ vinā pāpamocanaṁ na bhavati ca|
23 Kwa hiyo, ilikuwa muhimu kwa nakala za vitu vile vya mbinguni vitakaswe kwa dhabihu hizi, lakini vitu halisi vya mbinguni vilihitaji dhabihu bora kuliko hizi.
aparaṁ yāni svargīyavastūnāṁ dṛṣṭāntāsteṣām etaiḥ pāvanam āvaśyakam āsīt kintu sākṣāt svargīyavastūnām etebhyaḥ śreṣṭhe rbalidānaiḥ pāvanamāvaśyakaṁ|
24 Kwa maana Kristo hakuingia kwenye patakatifu palipofanywa kwa mikono ya mwanadamu, ambao ni mfano wa kile kilicho halisi. Yeye aliingia mbinguni penyewe, ili sasa aonekane mbele za Mungu kwa ajili yetu.
yataḥ khrīṣṭaḥ satyapavitrasthānasya dṛṣṭāntarūpaṁ hastakṛtaṁ pavitrasthānaṁ na praviṣṭavān kintvasmannimittam idānīm īśvarasya sākṣād upasthātuṁ svargameva praviṣṭaḥ|
25 Wala hakuingia mbinguni ili apate kujitoa mwenyewe mara kwa mara, kama vile kuhani mkuu aingiavyo Patakatifu pa Patakatifu kila mwaka kwa damu ambayo si yake mwenyewe.
yathā ca mahāyājakaḥ prativarṣaṁ paraśoṇitamādāya mahāpavitrasthānaṁ praviśati tathā khrīṣṭena punaḥ punarātmotsargo na karttavyaḥ,
26 Ingekuwa hivyo, ingempasa Kristo kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Lakini sasa ametokea mara moja tu katika mwisho wa nyakati aiondoe dhambi kwa kujitoa mwenyewe kuwa dhabihu. (aiōn )
karttavye sati jagataḥ sṛṣṭikālamārabhya bahuvāraṁ tasya mṛtyubhoga āvaśyako'bhavat; kintvidānīṁ sa ātmotsargeṇa pāpanāśārtham ekakṛtvo jagataḥ śeṣakāle pracakāśe| (aiōn )
27 Kama vile mwanadamu alivyowekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu,
aparaṁ yathā mānuṣasyaikakṛtvo maraṇaṁ tat paścād vicāro nirūpito'sti,
28 vivyo hivyo Kristo alitolewa mara moja tu kuwa dhabihu ili azichukue dhambi za watu wengi. Naye atakuja mara ya pili, sio kuchukua dhambi, bali kuwaletea wokovu wale wanaomngoja kwa shauku.
tadvat khrīṣṭo'pi bahūnāṁ pāpavahanārthaṁ balirūpeṇaikakṛtva utsasṛje, aparaṁ dvitīyavāraṁ pāpād bhinnaḥ san ye taṁ pratīkṣante teṣāṁ paritrāṇārthaṁ darśanaṁ dāsyati|