< Wahebrania 9 >
1 Basi agano lile la kwanza lilikuwa na kanuni zake za kuabudu na pia patakatifu pake pa kidunia.
Linu ni haiba chilikani chamatangilo chiba kwina milao ya kulapela mane nichibaka chijolola chefasi.
2 Hema ilitengenezwa. Katika sehemu yake ya kwanza kulikuwa na kinara cha taa, meza na mikate iliyowekwa wakfu; hii sehemu iliitwa Mahali Patakatifu.
Aho i tabenakele iba lukiswe. Chibaka camatangilo, mwi tabenakele, mubakwina matomeno e lambi, i ntafule, chinkwa cha kuba, chibali kusumpwa chibaka chijolola.
3 Nyuma ya pazia la pili, palikuwa na sehemu iliyoitwa Patakatifu pa Patakatifu,
Kwishilya lya majila abubeli akuhanzika kubena chimwi chibaka, chisumpwa chibaka chijolola ahulu.
4 ambapo palikuwa na yale madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba, na lile Sanduku la Agano lililofunikwa kwa dhahabu. Sanduku hili lilikuwa na gudulia la dhahabu lenye mana, ile fimbo ya Aroni iliyochipuka, na vile vibao vya mawe vya Agano.
Chibakwina katala ke gauda ka insense. Hape mubakwina i aleka ya chilikani, chibaku lamitwe chokuizula ni gauda. Mukati kayo kubena kapali mubena maana, inkoli ya Aroni iba tumpite, ni matapa a mabwe a chilikani.
5 Juu ya lile Sanduku kulikuwa na makerubi ya Utukufu yakitilia kivuli kile kifuniko ambacho ndicho kiti cha rehema. Lakini hatuwezi kueleza vitu hivi kwa undani sasa.
He uulu lye aleka ya chilikani, mashurubime ekanya a bwikilize chifupi cha kubolinsana hamwina, chitusawoli kuwamba hanu chakwizula.
6 Basi vitu hivi vilipokuwa vimepangwa, makuhani waliingia daima katika sehemu ya kwanza ya hema ili kufanya taratibu zao za ibada.
Hakumana ku bakanywa izizintu, ba purisita inako yonse babali kwinjila muchibaka chakunze che tabenakele kutenda mitendo yabo.
7 Lakini ni kuhani mkuu peke yake aliyeingia ndani ya sehemu ya pili ya hema. Tena hii ilikuwa mara moja tu kwa mwaka, na hakuingia kamwe bila damu, ambayo alitoa kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi za watu walizotenda bila kukusudia.
Kono kwanda a mupurisita yohanzi njabali kuwola kwinjila kuchibaka cha bubeli kamwina muchilimo, mi isiñi nikusena malaha aba lichitili chitabelo iye mwine mane nibantu baba tendi zibe isi chakulikeza.
8 Kwa njia hii, Roho Mtakatifu alikuwa anaonyesha kwamba, maadamu ile hema ya kwanza ilikuwa bado imesimama, njia ya kuingia Patakatifu pa Patakafifu ilikuwa bado haijafunguliwa.
Luhuho lujolola luba bonisi kuti inzila iya muchibaka chijolola ahulu kena ibeni ku patululwa kubona fela itabanakele ya tanzi ibakusi zimene.
9 Huu ulikuwa mfano kwa ajili ya wakati wa sasa, kuonyesha kwamba sadaka na dhabihu zilizokuwa zikitolewa hazikuweza kusafisha dhamiri ya mtu anayeabudu.
Ichi chibali chisupo che inu inako. zonse impo ni zitabelo zikwete kuhewa lyahanu kaziwoli ku shiyamisa sinte minahano ya balapeli.
10 Lakini hizi zilishughulika tu na vyakula na vinywaji, pamoja na taratibu mbalimbali za kunawa kwa nje, kanuni kwa ajili ya mwili zilizowekwa hadi wakati utimie wa matengenezo mapya.
Batwalize bulyo muhupulo kuzilyo ni kunywa mane nizimwi zintu zishelana shelana za mikiti ya kushanza. Iyi yonse ibali milao chenyama iba helwe kusikila intaelo inhya hete ni babumbwa.
11 Kristo alipokuja akiwa Kuhani Mkuu wa mambo mema ambayo tayari yameshawasili, alipitia kwenye hema iliyo kuu zaidi na bora zaidi, ambayo haikutengenezwa kwa mikono ya binadamu, hii ni kusema, ambayo si sehemu ya uumbaji huu.
Krisite abezi nali muprisita mukulwana wazintu zi lotu zibezi. Abenjili che tabenakele i nkando ni kushiyama ahulu isena iba tendwa chamayanza abantu, iyo isali ye fasi libabumbwa.
12 Hakuingia kwa njia ya damu ya mbuzi na ya ndama; lakini aliingia Patakatifu pa Patakatifu mara moja tu kwa damu yake mwenyewe, akiisha kupata ukombozi wa milele. (aiōnios )
Kahena ibali cha malaha empene ni a manamani, kono chamalaha akwe mwine abe njili limwina muchibaka chijolola ahulu ni kubukeleza ku uliwa kwetu kwa kuyakwile. (aiōnios )
13 Damu ya mbuzi na ya mafahali, na majivu ya mitamba walivyonyunyiziwa wale waliokuwa najisi kwa taratibu za kiibada viliwatakasa, hata kuwaondolea uchafu wa nje.
Kono haiba malaha empene ni ba mpho mi ni kusansela kwe twe lye nkomwana ya citole habo bababi nikwe awola kuba kungwila kwa Ireeza chakuba joloza mwi nyama,
14 Basi ni zaidi aje damu ya Kristo, ambaye kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na waa, itatusafisha dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo mauti, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai! (aiōnios )
mukusike hi chamalaha aKrisite, iye chaluuho lwakuya kusamani aba liihi mwine nikusena chinyansahala kwa Ireeza, kushanza maano etu kumitendo ifwile kutendela Ireeza yo hala? (aiōnios )
15 Kwa sababu hii Kristo ni mpatanishi wa agano jipya, ili kwamba wale walioitwa waweze kupokea ile ahadi ya urithi wa milele: kwa vile yeye alikufa awe ukombozi wao kutoka kwa dhambi walizozitenda chini ya agano la kwanza. (aiōnios )
Ka cheli ibaka, muzimanini wachilkani chihya. kwina bulyo nji kuti, kuzwa ifu haliba hindi chibaka chaku sumununa abo babena muchilikani chamatangilo kuzwa muzibe zabo, bana ba sumpitwe muba tambule insepiso yakuyola kwa kuya kusamani. (aiōnios )
16 Kwa habari ya wosia, ni muhimu kuthibitisha kifo cha yule aliyeutoa,
Aho hena iñolo lye nkabelo, ifu lya muntu yaba itendi liswanela ku bonekiswa.
17 kwa sababu wosia huwa na nguvu tu wakati mtu ameshakufa; kamwe hauwezi kutumika wakati yule aliyeuandika bado yuko hai.
Mukuti iñolo lyenkabelo li boniswa bulyo haiba chikwaba nifu, kakuti kalina maata haiba walitenda nasihala.
18 Hii ndiyo sababu hata lile agano la kwanza halikuweza kutekelezwa pasipo damu.
Mane nihaiba cilikani ca matangilo kena ciba bumbwa ni kusena malaha.
19 Mose alipotangaza kila amri kwa watu wote, alichukua damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji, sufu nyekundu na matawi ya mti wa hisopo, akanyunyizia kile kitabu na watu wote.
Mi mukuti Mushe haha intaelo ya mulao kubantu bonse, abahindi malaha amanamani ni impene, ni menzi, bwanda busubila, ni haisopa ni kusansela iñolo lye pampili ilee mane ni bantu bonse.
20 Alisema, “Hii ndiyo damu ya agano, ambalo Mungu amewaamuru kulitii.”
Kuzwaho nati, “Aa malaha acilikani awo Ireeza aba laeli kwenu.”
21 Vivyo hivyo alinyunyizia damu hiyo kwenye ile hema pamoja na kila kifaa kilichotumika ndani yake kwa taratibu za ibada.
Mwinzila iswana, aba sanseli malaha he tabenakele mane ni ha zi belekiso zonse zibali kutendiswa mwi nsebelezo.
22 Kwa kweli sheria hudai kwamba, karibu kila kitu kitakaswe kwa damu, wala pasipo kumwaga damu, hakuna msamaha wa dhambi.
Chakuya chamulawo, mukuti bungi bwa zintu zi ba kujolozwa cha malaha. Chikusena kwitila kwamalaha kakwina inswalelo.
23 Kwa hiyo, ilikuwa muhimu kwa nakala za vitu vile vya mbinguni vitakaswe kwa dhabihu hizi, lakini vitu halisi vya mbinguni vilihitaji dhabihu bora kuliko hizi.
Kuzwaaho kuba kuswanela kuti zintu zikola ubu zamwi wulu zi jolozwe hamwina ni zitabelo za zinyolozi. Nihakuba bulyo, zintu zamwi wulu zine zi swanela kujolozwa nenza ahulu kazitabelo sakata.
24 Kwa maana Kristo hakuingia kwenye patakatifu palipofanywa kwa mikono ya mwanadamu, ambao ni mfano wa kile kilicho halisi. Yeye aliingia mbinguni penyewe, ili sasa aonekane mbele za Mungu kwa ajili yetu.
Mukuti Kresite kana abenjili muchibaka chijolola ahulu chiba tendwa ni mayanza, icho chiswaniswo bulyo chache initi. Kusibulyo abenjili mwi wulu line, kuti hanu ali bonekise mwa Ireeza kwetu.
25 Wala hakuingia mbinguni ili apate kujitoa mwenyewe mara kwa mara, kama vile kuhani mkuu aingiavyo Patakatifu pa Patakatifu kila mwaka kwa damu ambayo si yake mwenyewe.
Kena abayi kwateni kuti akalinele tungi tungi, ubu mwabakutendela muprisita mukulwana, ya ba kwinjila muchibaka chijolola ahulu chilimo ni chilimo ni malaha achimwi.
26 Ingekuwa hivyo, ingempasa Kristo kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Lakini sasa ametokea mara moja tu katika mwisho wa nyakati aiondoe dhambi kwa kujitoa mwenyewe kuwa dhabihu. (aiōn )
Kambe mu kubekalile bulyo, linu ni kubaswaneli kuti anyande tungi tungi kuzwa kuma tangilo a mutomo we nkanda. Kono hanu inako imwina bulyo ku ma manimani azilimo zaba sinulwilwa kuti azwise chibe cha chitabelo chakwe mwine. (aiōn )
27 Kama vile mwanadamu alivyowekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu,
Zumwi ni zumwi ubikilwe kufwa limwina, mikuzwa aho kwiza i nkatulo.
28 vivyo hivyo Kristo alitolewa mara moja tu kuwa dhabihu ili azichukue dhambi za watu wengi. Naye atakuja mara ya pili, sio kuchukua dhambi, bali kuwaletea wokovu wale wanaomngoja kwa shauku.
Mwinzila iswana, Kresite naye, yaba neelwa limwina ku zwisa zibe za bangi, mwaboneke lwa bubeli, isi chakubonana nichibi, kono chempuluso yabana baba mulindili chenkulo inde.