< Wahebrania 9 >

1 Basi agano lile la kwanza lilikuwa na kanuni zake za kuabudu na pia patakatifu pake pa kidunia.
Hmaloe e lawkkamnae dawk hai bawknae phungnaw hoi talai van kaawm e kathounge hmuen ao.
2 Hema ilitengenezwa. Katika sehemu yake ya kwanza kulikuwa na kinara cha taa, meza na mikate iliyowekwa wakfu; hii sehemu iliitwa Mahali Patakatifu.
Bangkongtetpawiteh, lukkareiim a sak awh navah, kathounge hmuen tie ahmaloe e rakhan dawkvah, hmaiimkhok, caboi hoi vaiyeinaw a ta awh.
3 Nyuma ya pazia la pili, palikuwa na sehemu iliyoitwa Patakatifu pa Patakatifu,
Apâhni e yaphni athunglah teh hmuen kathoung poung telah kaw e rakhan ao.
4 ambapo palikuwa na yale madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba, na lile Sanduku la Agano lililofunikwa kwa dhahabu. Sanduku hili lilikuwa na gudulia la dhahabu lenye mana, ile fimbo ya Aroni iliyochipuka, na vile vibao vya mawe vya Agano.
Hote lukkareiim dawkvah, sui tongben hoi sui hoi sak e lawkkam thingkong ao. Hote thingkong dawk mana tanae sui hlaam, a pei ka pei e Aron e sonron, hoi kâlawk thutnae lungphennaw ao.
5 Juu ya lile Sanduku kulikuwa na makerubi ya Utukufu yakitilia kivuli kile kifuniko ambacho ndicho kiti cha rehema. Lakini hatuwezi kueleza vitu hivi kwa undani sasa.
Hote thingkong van vah, ka lentoe e cherubim ni yonthanae hmuen hah a ramuk. Hote hnonaw teh atu ka kamceng lah dei thai lah awmhoeh.
6 Basi vitu hivi vilipokuwa vimepangwa, makuhani waliingia daima katika sehemu ya kwanza ya hema ili kufanya taratibu zao za ibada.
Hottelah, hnonaw pueng koung rakueng awh torei teh, vaihmanaw teh lukkareiim apasuek e rakhan thungvah bawknae thawnaw tawk hanlah atu hoi atu a kâen awh.
7 Lakini ni kuhani mkuu peke yake aliyeingia ndani ya sehemu ya pili ya hema. Tena hii ilikuwa mara moja tu kwa mwaka, na hakuingia kamwe bila damu, ambayo alitoa kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi za watu walizotenda bila kukusudia.
Apâhni e rakhan dawk teh vaihma kacue ni dueng doeh kum touh dawk vai touh ouk a kâen. Hottelah a kâen navah ama han hoi taminaw ni yon a sak payonnae hanlah thoseh, thueng nahanlah thi hoi ouk a kâen.
8 Kwa njia hii, Roho Mtakatifu alikuwa anaonyesha kwamba, maadamu ile hema ya kwanza ilikuwa bado imesimama, njia ya kuingia Patakatifu pa Patakafifu ilikuwa bado haijafunguliwa.
Lukkareiim apasueke rakhan ao roukrak, kathoungpounge rakhan koe kâen thainae lam aw hoeh rah tie hah Kathoung Muitha ni hete hno hoi a pâpho.
9 Huu ulikuwa mfano kwa ajili ya wakati wa sasa, kuonyesha kwamba sadaka na dhabihu zilizokuwa zikitolewa hazikuweza kusafisha dhamiri ya mtu anayeabudu.
Hote teh, atutueng hanelah bangnuenae lah a o. Thuengnae poehnonaw hoi thueng e satheinaw ni mahoima kâpanuenae lung thoungsak thai hoeh.
10 Lakini hizi zilishughulika tu na vyakula na vinywaji, pamoja na taratibu mbalimbali za kunawa kwa nje, kanuni kwa ajili ya mwili zilizowekwa hadi wakati utimie wa matengenezo mapya.
Hote hnonaw teh canei kawi hoi kâpasunae phungnaw hoi a kâkuet teh, a katha lah bout sak hoehnahlan totouh takthai hoi kâkuen e phunglam lah doeh ao.
11 Kristo alipokuja akiwa Kuhani Mkuu wa mambo mema ambayo tayari yameshawasili, alipitia kwenye hema iliyo kuu zaidi na bora zaidi, ambayo haikutengenezwa kwa mikono ya binadamu, hii ni kusema, ambayo si sehemu ya uumbaji huu.
Hatei, Khrih teh hno kahawinaw hoi kâkuen e Vaihma Kacue lahoi a tho toung dawkvah, tami kut hoi sak e nahoeh, het talai van e nahoeh, hoe ka lentoe niteh hoe kakuep e lukkareiim dawkvah,
12 Hakuingia kwa njia ya damu ya mbuzi na ya ndama; lakini aliingia Patakatifu pa Patakatifu mara moja tu kwa damu yake mwenyewe, akiisha kupata ukombozi wa milele. (aiōnios g166)
Hmae hoi Maitoca e thipaling tho laipalah amae thi roeroe a sin teh kathoungpounge hmuen koe a kâen teh maimouh han lah a yungyoe ratangnae vaitahoi kakhoutlah a sak toe. (aiōnios g166)
13 Damu ya mbuzi na ya mafahali, na majivu ya mitamba walivyonyunyiziwa wale waliokuwa najisi kwa taratibu za kiibada viliwatakasa, hata kuwaondolea uchafu wa nje.
Bangkongtetpawiteh, kathounghoehe taminaw van vah kahei e maito thi, hmae thi hoi Maitola sawi e hraba ni ahnimae takthai dawk thoungsak thai boipawiteh,
14 Basi ni zaidi aje damu ya Kristo, ambaye kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na waa, itatusafisha dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo mauti, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai! (aiōnios g166)
a yungyoe Muitha lahoi yah yonnae ka tawn hoeh e amahoima Cathut koe ka kâthueng e Khrih e a thipaling teh kahring Cathut thaw tawk thai nahanelah, nangmae thoehawi panuenae lungthin duenae tawksaknae thung hoi hoe thoungsak thai mahoeh namaw. (aiōnios g166)
15 Kwa sababu hii Kristo ni mpatanishi wa agano jipya, ili kwamba wale walioitwa waweze kupokea ile ahadi ya urithi wa milele: kwa vile yeye alikufa awe ukombozi wao kutoka kwa dhambi walizozitenda chini ya agano la kwanza. (aiōnios g166)
Hatdawkvah, hmaloe e lawkkam rahim yonnae dawk hoi hlout sak hanlah, Khrih teh a due toung dawkvah, a kaw e naw ni yungyoe râw hah a coe thai awh nahanlah Bawipa teh lawkkam katha e laicei lah ao. (aiōnios g166)
16 Kwa habari ya wosia, ni muhimu kuthibitisha kifo cha yule aliyeutoa,
Râw coenae lawk teh râw coenae lawk kadeikung a due hnukkhu to doeh ouk a coe awh.
17 kwa sababu wosia huwa na nguvu tu wakati mtu ameshakufa; kamwe hauwezi kutumika wakati yule aliyeuandika bado yuko hai.
Bangkongtetpawiteh lawk kadeikung a hring nathung teh cungkei hoeh, a due hnukkhu torei doeh to e lah ao.
18 Hii ndiyo sababu hata lile agano la kwanza halikuweza kutekelezwa pasipo damu.
Hatdawkvah, hmaloe e lawkkamnae haiyah thipaling laipalah sak hoeh.
19 Mose alipotangaza kila amri kwa watu wote, alichukua damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji, sufu nyekundu na matawi ya mti wa hisopo, akanyunyizia kile kitabu na watu wote.
Mosi ni kâlawk cauk dawk kaawm e kâlawknaw pueng hah rangpuinaw koe a pathang pouh hnukkhu, tui hoi kalawt e maito hoi hmae thi hah a sin teh tumuen paling hoi dingsala dawn hoi kâlawk cauk hoi rangpuinaw hah a kahei sin.
20 Alisema, “Hii ndiyo damu ya agano, ambalo Mungu amewaamuru kulitii.”
Hete thi teh, Cathut ni nangmouh koe kâ a poe e lawkkamnae thipaling doeh a ti.
21 Vivyo hivyo alinyunyizia damu hiyo kwenye ile hema pamoja na kila kifaa kilichotumika ndani yake kwa taratibu za ibada.
Hathnukkhu hot patetvanlah, lukkareiim hoi bawknae koe hno e hnopainaw lathueng hai thipaling a kahei sin.
22 Kwa kweli sheria hudai kwamba, karibu kila kitu kitakaswe kwa damu, wala pasipo kumwaga damu, hakuna msamaha wa dhambi.
Kâlawk patetlah bangpuengpa heh thipaling hoi thoungsak thai lah ao. Thi palawng laipalah yon ngaithoumnae awmhoeh.
23 Kwa hiyo, ilikuwa muhimu kwa nakala za vitu vile vya mbinguni vitakaswe kwa dhabihu hizi, lakini vitu halisi vya mbinguni vilihitaji dhabihu bora kuliko hizi.
Kalvanlae hnonaw e tâhlipnaw hah hottelah thuengnae lahoi thoungsak lah ao teh, kalvan lae hnonaw hateh hoe ka talue e thuengnae lahoi thoungsak lah ao.
24 Kwa maana Kristo hakuingia kwenye patakatifu palipofanywa kwa mikono ya mwanadamu, ambao ni mfano wa kile kilicho halisi. Yeye aliingia mbinguni penyewe, ili sasa aonekane mbele za Mungu kwa ajili yetu.
Bangkongtetpawiteh, Khrih teh a katang e hmuen kathoungpounge tâhlip lah kaawm e tami ni kut hoi sak e kathoungpounge hmuen dawk kâen hoeh, maimouh han kecu dawk atu Cathut e a hmalah amahoima kâpâtue hanlah kalvan vah a kâen toe.
25 Wala hakuingia mbinguni ili apate kujitoa mwenyewe mara kwa mara, kama vile kuhani mkuu aingiavyo Patakatifu pa Patakatifu kila mwaka kwa damu ambayo si yake mwenyewe.
Vaihma kacue ni sathei thi sin laihoi kum tangkuem kathoungpounge hmuen koe a kâen e patetlah Khrih teh a mahoima atuhoitu thueng hanelah panki hoeh.
26 Ingekuwa hivyo, ingempasa Kristo kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Lakini sasa ametokea mara moja tu katika mwisho wa nyakati aiondoe dhambi kwa kujitoa mwenyewe kuwa dhabihu. (aiōn g165)
Hottelah hoehpawiteh, talaivan a paw pasuek hoi avai moikapap a khang han doeh toe. Atuteh a tue abawnae koe lah a mahoima vai touh thuengnae lahoi yon thoungsak hanlah a tho toe. (aiōn g165)
27 Kama vile mwanadamu alivyowekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu,
Tami teh vai touh due hnukkhu lawkcengnae a kâhmo e patetlah,
28 vivyo hivyo Kristo alitolewa mara moja tu kuwa dhabihu ili azichukue dhambi za watu wengi. Naye atakuja mara ya pili, sio kuchukua dhambi, bali kuwaletea wokovu wale wanaomngoja kwa shauku.
Khrih ni taminaw e yonnaw ceikhai hanelah, amahoima vai touh dueng thuengnae a sak teh, apâhni e dawk teh yon hoi kâkuen laipalah, rungngangnae kangaihawinaw han lah apâhni bout a kum han.

< Wahebrania 9 >