< Wahebrania 8 >

1 Basi jambo tunalotaka kulisema ni hili: Tunaye Kuhani Mkuu ambaye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Aliye Mkuu mbinguni,
Or l'abrégé de notre discours, [c'est que] nous avons un tel souverain Sacrificateur qui est assis à la droite du trône de la Majesté [de Dieu] dans les Cieux,
2 yeye ahudumuye katika patakatifu, hema la kweli lililowekwa na Bwana, wala si na mwanadamu.
Ministre du Sanctuaire, et du vrai Tabernacle, que le Seigneur a dressé et non pas les hommes.
3 Kila kuhani mkuu huwekwa ili atoe sadaka na dhabihu. Vivyo hivyo, ilikuwa jambo muhimu kwa huyu Kuhani naye awe na kitu cha kutoa.
Car tout souverain Sacrificateur est ordonné pour offrir des dons et des sacrifices, c'est pourquoi il est nécessaire que celui-ci aussi ait eu quelque chose pour offrir.
4 Kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani, kwa sababu tayari wapo watu watoao sadaka kama ilivyoelekezwa na sheria.
Vu même que s'il était sur la terre il ne serait pas Sacrificateur, pendant qu'il y aurait des Sacrificateurs qui offrent des dons selon la Loi;
5 Wanahudumu katika patakatifu palipo mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni. Hii ndiyo sababu Mose alionywa alipokaribia kujenga hema, akiambiwa: “Hakikisha kuwa unavitengeneza vitu vyote kwa mfano ulioonyeshwa kule mlimani.”
Lesquels font le service dans le lieu qui n'est que l'image et l'ombre des choses célestes, selon que Dieu le dit à Moïse, quand il devait achever le Tabernacle: Or prends garde, lui dit-il, de faire toutes choses selon le modèle qui t'a été montré sur la montagne.
6 Lakini huduma aliyopewa Yesu ni bora zaidi kuliko yao, kama vile agano ambalo yeye ni mpatanishi wake lilivyo bora zaidi kuliko lile la zamani, nalo limewekwa misingi wa ahadi zilizo bora zaidi.
Mais maintenant [notre souverain Sacrificateur] a obtenu un ministère d'autant plus excellent, qu'il est Médiateur d'une plus excellente alliance, qui est établie sous de meilleures promesses.
7 Kwa maana kama hapakuwa na kasoro katika lile agano la kwanza, pasingekuwa na haja ya kutafuta nafasi kwa ajili ya jingine.
Parce que s'il n'y eût eu rien à redire dans la première, il n'eût jamais été cherché de lieu à une seconde.
8 Lakini Mungu aliona kosa kwa watu, naye akasema: “Siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.
Car en censurant [les Juifs, Dieu] leur dit: Voici, les jours viendront, dit le Seigneur, que je traiterai avec la maison d'Israël et avec la maison de Juda une Nouvelle alliance:
9 Agano langu halitakuwa kama lile nililofanya na baba zao nilipowashika mkono kuwaongoza watoke nchi ya Misri, kwa sababu hawakuendelea kuwa waaminifu katika agano langu, nami nikawaacha, asema Bwana.
Non selon l'alliance que je traitai avec leurs pères, le jour que je les pris par la main pour les tirer du pays d'Egypte, car ils n'ont point persévéré dans mon alliance; c'est pourquoi je les ai méprisés, dit le Seigneur.
10 Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku zile, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu katika nia zao na kuziandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Mais voici l'alliance que je traiterai après ces jours-là avec la maison d'Israël, dit le Seigneur, [c'est que] je mettrai mes lois dans leur entendement, et je les écrirai dans leur cœur; et je serai leur Dieu, et ils seront mon peuple.
11 Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana,’ kwa sababu wote watanijua mimi, tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana.
Et chacun n'enseignera point son prochain, ni chacun son frère, en disant: connais le Seigneur; parce qu'ils me connaîtront tous, depuis le plus petit jusqu'au plus grand d'entre eux.
12 Kwa sababu nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”
Car je serai apaisé par rapport à leurs injustices, et je ne me souviendrai plus de leurs péchés, ni de leurs iniquités.
13 Kwa kuliita agano hili “jipya,” Mungu amefanya lile agano la kwanza kuwa kuukuu; nacho kitu kinachoanza kuchakaa na kuwa kikuukuu kiko karibu kutoweka.
En disant une nouvelle [alliance], il envieillit la première: or, ce qui devient vieux et ancien, est près d'être aboli.

< Wahebrania 8 >