< Wahebrania 6 >
1 Kwa hiyo, tukiachana na mafundisho yale ya awali kuhusu Kristo na tukisonga mbele ili tufikie utimilifu, sio kuweka tena msingi wa mafundisho ya kuzitubia kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,
Therefore leaving elementary instruction about the Christ, let us advance to mature manhood and not be continually re-laying a foundation of repentance from lifeless works and of faith in God,
2 mafundisho kuhusu aina za ubatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. (aiōnios )
or of teaching about ceremonial washings, the laying on of hands, the resurrection of the dead, and the last judgement. (aiōnios )
3 Mungu akitujalia tutafanya hivyo.
And advance we will, if God permits us to do so.
4 Kwa kuwa ni vigumu kwa wale ambao wakati fulani walishapata nuru, ambao walishaonja kipawa cha mbinguni, ambao wamekwisha kushiriki katika Roho Mtakatifu,
For it is impossible, in the case of those who have once for all been enlightened, and have tasted the sweetness of the heavenly gift, and have been made partakers of the Holy Spirit,
5 ambao wameonja uzuri wa Neno la Mungu na nguvu za wakati ujao, (aiōn )
and have realized how good the word of God is and how mighty are the powers of the coming Age, and then fell away-- (aiōn )
6 kisha wakianguka, kuwarejesha tena katika toba. Kwa kuwa wanamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili na kumdhalilisha hadharani, nayo ikawa hasara kwao.
it is impossible, I say, to keep bringing them back to a new repentance, for, to their own undoing, they are repeatedly crucifying the Son of God afresh and exposing Him to open shame.
7 Ardhi ile ipokeayo mvua inyeshayo juu yake mara kwa mara hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao kwa ajili yao yalimwa, nayo nchi hiyo hupokea baraka kutoka kwa Mungu.
For land which has drunk in the rain that often falls upon it, and brings forth vegetation useful to those for whose sakes, indeed, it is tilled, has a share in God's blessing.
8 Lakini ardhi ikizaa miiba na mibaruti, haina thamani na iko hatarini ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.
But if it only yields a mass of thorns and briers, it is considered worthless, and is in danger of being cursed, and in the end will be destroyed by fire.
9 Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu wapendwa, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mema zaidi, mambo yale yahusuyo wokovu.
But we, even while we speak in this tone, have a happier conviction concerning you, my dearly-loved friends--a conviction of things which point towards salvation.
10 Mungu si mdhalimu: yeye hataisahau kazi yenu na upendo ule mlioonyesha kwa ajili yake katika kuwahudumia watakatifu na hata sasa mnaendelea kuwahudumia.
For God is not unjust so that He is unmindful of your labour and of the love which you have manifested towards Himself in having rendered services to His people and in still rendering them.
11 Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho,
But we long for each of you to continue to manifest the same earnestness, with a view to your enjoying fulness of hope to the very End;
12 ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.
so that you may not become half-hearted, but be imitators of those who through faith and patient endurance are now heirs to the promises.
13 Mungu alipompa Abrahamu ahadi yake, kwa kuwa hakuwepo mwingine aliyekuwa mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake, aliapa kwa nafsi yake,
For when God gave the promise to Abraham, since He had no one greater to swear by, He swore by Himself,
14 akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.”
saying, "Assuredly I will bless you and bless you, I will increase you and increase you."
15 Abrahamu naye, baada ya kungoja kwa saburi, alipokea kile kilichoahidiwa.
And so, as the result of patient waiting, our forefather obtained what God had promised.
16 Wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuwaliko, nacho kiapo hicho huthibitisha kile kilichosemwa na hivyo humaliza mabishano yote.
For men swear by what is greater than themselves; and with them an oath in confirmation of a statement always puts an end to a dispute.
17 Mungu alipotaka kuonyesha kwa udhahiri zaidi ile asili ya kutokubadilika kwa ahadi yake kwa warithi wa ahadi, aliithitibisha kwa kiapo.
In the same way, since it was God's desire to display more convincingly to the heirs of the promise how unchangeable His purpose was,
18 Mungu alifanya hivyo ili kwa vitu viwili visivyobadilika, yaani ahadi yake na kiapo chake, ambavyo kwavyo Mungu hawezi kusema uongo, sisi ambao tumemkimbilia ili tulishike lile tumaini lililowekwa mbele yetu tuwe na faraja thabiti.
He added an oath, in order that, through two unchangeable things, in which it is impossible for Him to prove false, we may possess mighty encouragement--we who, for safety, have hastened to lay hold of the hope set before us.
19 Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho iliyo imara na thabiti. Tumaini hili huingia katika sehemu takatifu iliyopo nyuma ya pazia,
That hope we have as an anchor of the soul--an anchor that can neither break nor drag. It passes in behind the veil,
20 mahali ambapo Yesu mtangulizi wetu aliingia kwa niaba yetu. Yeye amekuwa Kuhani Mkuu milele, kwa mfano wa Melkizedeki. (aiōn )
where Jesus has entered as a forerunner on our behalf, having become, like Melchizedek, a High Priest for ever. (aiōn )