< Wahebrania 6 >
1 Kwa hiyo, tukiachana na mafundisho yale ya awali kuhusu Kristo na tukisonga mbele ili tufikie utimilifu, sio kuweka tena msingi wa mafundisho ya kuzitubia kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,
Let us then, leaving the first principles of the doctrine of Christ, press on to perfection; not laying again the foundation of repentance from dead works, and of faith toward God,
2 mafundisho kuhusu aina za ubatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. (aiōnios )
of the doctrine of baptisms, and of the laying on of hands, and of resurrection of the dead, and of everlasting judgment. (aiōnios )
3 Mungu akitujalia tutafanya hivyo.
And this we will do, if God permit.
4 Kwa kuwa ni vigumu kwa wale ambao wakati fulani walishapata nuru, ambao walishaonja kipawa cha mbinguni, ambao wamekwisha kushiriki katika Roho Mtakatifu,
For it is impossible that those who have once been enlightened, and have tasted of the heavenly gift, and been make partakers of the Holy Spirit,
5 ambao wameonja uzuri wa Neno la Mungu na nguvu za wakati ujao, (aiōn )
and have tasted the good word of God, and the powers of the world to come, (aiōn )
6 kisha wakianguka, kuwarejesha tena katika toba. Kwa kuwa wanamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili na kumdhalilisha hadharani, nayo ikawa hasara kwao.
and have fallen away, should again be renewed to repentance, since they crucify to themselves the Son of God afresh, and put him to open shame.
7 Ardhi ile ipokeayo mvua inyeshayo juu yake mara kwa mara hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao kwa ajili yao yalimwa, nayo nchi hiyo hupokea baraka kutoka kwa Mungu.
For the earth which hath drunk in the rain that cometh often upon it, and beareth plants useful to those for whose sake it is tilled, receiveth blessing from God;
8 Lakini ardhi ikizaa miiba na mibaruti, haina thamani na iko hatarini ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.
but if it bear thorns and briers it is disapproved, and is near to being accursed; and its end is to be burned.
9 Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu wapendwa, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mema zaidi, mambo yale yahusuyo wokovu.
But, beloved, we are persuaded better things of you, and things that are connected with salvation, though we do thus speak.
10 Mungu si mdhalimu: yeye hataisahau kazi yenu na upendo ule mlioonyesha kwa ajili yake katika kuwahudumia watakatifu na hata sasa mnaendelea kuwahudumia.
For God is not unjust so as to forget your work, and the love which ye showed toward his name, in that ye ministered and are still ministering to the saints.
11 Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho,
But we earnestly desire that every one of you may show the same diligence with regard to the full assurance of your hope even to the end;
12 ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.
that ye may not become slothful, but imitators of those who through faith and endurance inherit the promises.
13 Mungu alipompa Abrahamu ahadi yake, kwa kuwa hakuwepo mwingine aliyekuwa mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake, aliapa kwa nafsi yake,
For when God made a promise to Abraham, since he could swear by no greater, he swore by himself,
14 akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.”
saying, “Surely blessing I will bless thee, and multiplying I will multiply thee.”
15 Abrahamu naye, baada ya kungoja kwa saburi, alipokea kile kilichoahidiwa.
And so, having endured with patience, he obtained the promised blessing.
16 Wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuwaliko, nacho kiapo hicho huthibitisha kile kilichosemwa na hivyo humaliza mabishano yote.
For men indeed swear by one who is greater, and the oath for confirmation is to them an end of all strife.
17 Mungu alipotaka kuonyesha kwa udhahiri zaidi ile asili ya kutokubadilika kwa ahadi yake kwa warithi wa ahadi, aliithitibisha kwa kiapo.
Wherefore God, wishing more abundantly to show to the heirs of the promise the immutability of his purpose, confirmed it by an oath,
18 Mungu alifanya hivyo ili kwa vitu viwili visivyobadilika, yaani ahadi yake na kiapo chake, ambavyo kwavyo Mungu hawezi kusema uongo, sisi ambao tumemkimbilia ili tulishike lile tumaini lililowekwa mbele yetu tuwe na faraja thabiti.
that by two immutable things, in which it is impossible for God to lie, we may have strong encouragement, who have fled for refuge to lay hold upon the hope set before us;
19 Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho iliyo imara na thabiti. Tumaini hili huingia katika sehemu takatifu iliyopo nyuma ya pazia,
which hope we have as an anchor of the soul, sure and steadfast, and which entereth within the veil;
20 mahali ambapo Yesu mtangulizi wetu aliingia kwa niaba yetu. Yeye amekuwa Kuhani Mkuu milele, kwa mfano wa Melkizedeki. (aiōn )
where as forerunner for us Jesus entered, having become a high-priest for ever, after the order of Melchizedek. (aiōn )