< Wahebrania 5 >

1 Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa wanadamu anawekwa kuwawakilisha kwa mambo yanayomhusu Mungu, ili apate kutoa matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For every high priest, being taken from amongst men, is appointed for men in things pertaining to God, that he may offer both gifts and sacrifices for sins.
2 Kwa kuwa yeye mwenyewe ni dhaifu, aweza kuwachukulia kwa upole wale wasiojua na kupotoka.
The high priest can deal gently with those who are ignorant and going astray, because he himself is also surrounded with weakness.
3 Hii ndiyo sababu inampasa kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na vivyo hivyo kwa ajili ya dhambi za watu.
Because of this, he must offer sacrifices for sins for the people, as well as for himself.
4 Hakuna anayejitwalia heshima hii mwenyewe; ni lazima aitwe na Mungu, kama vile Aroni alivyoitwa.
Nobody takes this honour on himself, but he is called by God, just like Aaron was.
5 Pia Kristo hakujitwalia utukufu yeye mwenyewe wa kuwa Kuhani Mkuu, bali Mungu alimwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.”
So also Messiah didn’t glorify himself to be made a high priest, but it was he who said to him, “You are my Son. Today I have become your father.”
6 Pia mahali pengine asema, “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.” (aiōn g165)
As he says also in another place, “You are a priest forever, after the order of Melchizedek.” (aiōn g165)
7 Katika siku za maisha ya Yesu hapa duniani, alimtolea maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, yeye awezaye kumwokoa na mauti, naye Mungu akamsikia kwa sababu ya kutii kwake kwa unyenyekevu.
He, in the days of his flesh, having offered up prayers and petitions with strong crying and tears to him who was able to save him from death, and having been heard for his godly fear,
8 Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza utiifu kutokana na mateso aliyoyapata,
though he was a Son, yet learnt obedience by the things which he suffered.
9 na akiisha kukamilishwa, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii. (aiōnios g166)
Having been made perfect, he became to all of those who obey him the author of eternal salvation, (aiōnios g166)
10 Naye amewekwa na Mungu kuwa Kuhani Mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
named by God a high priest after the order of Melchizedek.
11 Tunayo mengi ya kusema kuhusu habari ya ukuhani huu, lakini ni vigumu kuyaeleza, kwa sababu ninyi ni wazito wa kuelewa.
About him we have many words to say, and hard to interpret, seeing you have become dull of hearing.
12 Kwa hakika, ingawa mpaka wakati huu ingewapasa kuwa walimu, bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za awali za kweli ya Neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu!
For although by this time you should be teachers, you again need to have someone teach you the rudiments of the first principles of the revelations of God. You have come to need milk, and not solid food.
13 Kwa maana yeyote aishiye kwa kunywa maziwa bado yeye ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafundisho kuhusu neno la haki.
For everyone who lives on milk is not experienced in the word of righteousness, for he is a baby.
14 Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ambao kwa kujizoeza wamejifunza kupambanua kati ya mema na mabaya.
But solid food is for those who are full grown, who by reason of use have their senses exercised to discern good and evil.

< Wahebrania 5 >