< Wahebrania 5 >

1 Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa wanadamu anawekwa kuwawakilisha kwa mambo yanayomhusu Mungu, ili apate kutoa matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi.
Now every high priest taken from among men is appointed to act on behalf of men in things pertaining to God, that he may offer both gifts and sacrifices for sins,
2 Kwa kuwa yeye mwenyewe ni dhaifu, aweza kuwachukulia kwa upole wale wasiojua na kupotoka.
being able to deal gently with those who sin in ignorance and go astray, since he himself is also subject to weakness.
3 Hii ndiyo sababu inampasa kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na vivyo hivyo kwa ajili ya dhambi za watu.
Because of this he must offer sacrifices for his own sins as well, just as he does for the people's.
4 Hakuna anayejitwalia heshima hii mwenyewe; ni lazima aitwe na Mungu, kama vile Aroni alivyoitwa.
Also, no one receives this honor on his own, but upon being called by God, just like Aaron.
5 Pia Kristo hakujitwalia utukufu yeye mwenyewe wa kuwa Kuhani Mkuu, bali Mungu alimwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.”
So also Christ did not exalt Himself to become High Priest, but it was He[F] who said to Him[S], “You are my Son; today I have begotten You.”
6 Pia mahali pengine asema, “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.” (aiōn g165)
Just as He[F] also says in another place, “You are a priest forever according to the order of Melchizedek.” (aiōn g165)
7 Katika siku za maisha ya Yesu hapa duniani, alimtolea maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, yeye awezaye kumwokoa na mauti, naye Mungu akamsikia kwa sababu ya kutii kwake kwa unyenyekevu.
He[S], in the days of His flesh, having offered up both prayers and supplications, with a loud cry and tears, to the One who was able to save Him from death, and having been answered because of His godly fear,
8 Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza utiifu kutokana na mateso aliyoyapata,
although being SON, He learned obedience by the things which He suffered.
9 na akiisha kukamilishwa, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii. (aiōnios g166)
And having been completed He became the Source of eternal salvation for all those obeying Him, (aiōnios g166)
10 Naye amewekwa na Mungu kuwa Kuhani Mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
having been designated by God as High Priest ‘according to the order of Melchizedek’;
11 Tunayo mengi ya kusema kuhusu habari ya ukuhani huu, lakini ni vigumu kuyaeleza, kwa sababu ninyi ni wazito wa kuelewa.
concerning whom we have much to say, but it is hard to explain, since you have become sluggish in hearing.
12 Kwa hakika, ingawa mpaka wakati huu ingewapasa kuwa walimu, bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za awali za kweli ya Neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu!
Really, because although by this time you ought to be teachers, you need someone to teach you the elementary principles of God's oracles all over again; you have come to the point of needing milk, not solid food!
13 Kwa maana yeyote aishiye kwa kunywa maziwa bado yeye ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafundisho kuhusu neno la haki.
Surely; whoever lives on milk is an infant, and therefore unskilled in the Word of righteousness.
14 Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ambao kwa kujizoeza wamejifunza kupambanua kati ya mema na mabaya.
On the other hand, solid food is for the mature, those who by habitual use have trained their senses to distinguish good from bad.

< Wahebrania 5 >