< Wahebrania 4 >
1 Kwa hiyo, kwa kuwa bado ahadi ya kuingia rahani iko wazi, tujihadhari ili hata mmoja wenu asije akaikosa.
Let us therefore fear, lest a promise being left [us] of entering into his rest, any of you should seem to come short of it.
2 Kwa maana sisi pia tumesikia Injili iliyohubiriwa kwetu, kama nao walivyosikia; lakini ujumbe ule waliousikia haukuwa na maana kwao, kwa sababu wale waliousikia hawakuuchanganya na imani.
For to us was the gospel preached, as well as to them: but the word which they heard did not profit them, not being mixed with faith in them that heard [it].
3 Sasa sisi ambao tumeamini tunaingia katika ile raha, kama vile Mungu alivyosema, “Kwa hiyo nikaapa katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’” Lakini kazi yake ilikamilika tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
For we who have believed do enter into rest, as he said, As I have sworn in my wrath, if they shall enter into my rest: although the works were finished from the foundation of the world.
4 Kwa maana mahali fulani amezungumza kuhusu siku ya saba, akisema: “Katika siku ya saba Mungu alipumzika kutoka kazi zake zote.”
For he spoke in a certain place of the seventh [day] on this wise, And God rested the seventh day from all his works.
5 Tena hapo juu asema, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”
And in this [place] again, If they shall enter into my rest.
6 Kwa hiyo inabaki kuwa wazi kwa wengine kuingia, nao wale wa kwanza waliopokea Injili walishindwa kuingia kwa sababu ya kutokutii.
Seeing therefore it remaineth that some must enter into it, and they to whom it was first preached entered not because of unbelief:
7 Kwa hiyo Mungu ameweka siku nyingine, akaiita Leo, akisema kwa kinywa cha Daudi baadaye sana, kwa maneno yaliyotangulia kunenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu.”
(Again, he limiteth a certain day, saying in David, To-day, after so long a time; as it is said, To-day, if ye will hear his voice, harden not your hearts.
8 Kwa maana kama Yoshua alikuwa amewapa raha, Mungu hangesema tena baadaye kuhusu siku nyingine.
For if Jesus had given them rest, then he would not afterward have spoken of another day.
9 Kwa hiyo basi, imebaki raha ya Sabato kwa ajili ya watu wa Mungu;
There remaineth therefore a rest to the people of God.
10 kwa kuwa kila mmoja aingiaye katika raha ya Mungu pia hupumzika kutoka kazi zake mwenyewe, kama vile Mungu alivyopumzika kutoka kazi zake.
For he that hath entered into his rest, he also hath ceased from his own works, as God [did] from his.)
11 Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha hiyo, ili kwamba asiwepo yeyote atakayeanguka kwa kufuata mfano wao wa kutokutii.
Let us labor therefore to enter into that rest, lest any man fall after the same example of unbelief.
12 Kwa maana Neno la Mungu li hai tena lina nguvu. Lina makali kuliko upanga wowote wenye makali kuwili, hivyo linachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, viungo na mafuta yaliyo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
For the word of God [is] living, and powerful, and sharper than any two-edged sword, piercing even to the dividing asunder of soul and spirit, and of the joints and marrow, and [is] a discerner of the thoughts and intents of the heart.
13 Wala hakuna kiumbe chochote kilichofichika machoni pa Mungu. Kila kitu kimefunuliwa na kiko wazi machoni pake yeye ambaye kwake ni lazima tutatoa hesabu.
Neither is there any creature that is not manifest in his sight: but all things [are] naked and opened to the eyes of him with whom we have to do.
14 Kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu kuliko wote ambaye ameingia mbinguni, Yesu Mwana wa Mungu, basi na tushikamane sana kwa uthabiti na ule ukiri wa imani yetu.
Seeing then that we have a great High Priest, that hath passed into the heavens, Jesus the Son of God, let us hold fast [our] profession.
15 Kwa kuwa hatuna Kuhani Mkuu asiyeweza kuchukuliana na sisi katika udhaifu wetu, lakini tunaye mmoja ambaye alijaribiwa kwa kila namna, kama vile sisi tujaribiwavyo: lakini yeye hakutenda dhambi.
For we have not a high priest who cannot be touched with the feeling of our infirmities; but who was in all points tempted as [we are], [yet] without sin.
16 Basi na tukikaribie kiti cha rehema kwa ujasiri, ili tupewe rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.
Let us therefore come boldly to the throne of grace, that we may obtain mercy, and find grace to help in time of need.