< Wahebrania 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa bado ahadi ya kuingia rahani iko wazi, tujihadhari ili hata mmoja wenu asije akaikosa.
Let vs feare therefore, least at any time by forsaking the promise of entring into his rest, any of you should seeme to be depriued.
2 Kwa maana sisi pia tumesikia Injili iliyohubiriwa kwetu, kama nao walivyosikia; lakini ujumbe ule waliousikia haukuwa na maana kwao, kwa sababu wale waliousikia hawakuuchanganya na imani.
For vnto vs was the Gospel preached as also vnto them: but the worde that they heard, profited not them, because it was not mixed with faith in those that heard it.
3 Sasa sisi ambao tumeamini tunaingia katika ile raha, kama vile Mungu alivyosema, “Kwa hiyo nikaapa katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’” Lakini kazi yake ilikamilika tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
For we which haue beleeued, doe enter into rest, as he said to the other, As I haue sworne in my wrath, If they shall enter into my rest: although the workes were finished from the foundation of the world.
4 Kwa maana mahali fulani amezungumza kuhusu siku ya saba, akisema: “Katika siku ya saba Mungu alipumzika kutoka kazi zake zote.”
For he spake in a certaine place of the seuenth day on this wise, And God did rest the seuenth day from all his workes.
5 Tena hapo juu asema, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”
And in this place againe, If they shall enter into my rest.
6 Kwa hiyo inabaki kuwa wazi kwa wengine kuingia, nao wale wa kwanza waliopokea Injili walishindwa kuingia kwa sababu ya kutokutii.
Seeing therefore it remaineth that some must enter thereinto, and they to whom it was first preached, entred not therein for vnbeliefes sake:
7 Kwa hiyo Mungu ameweka siku nyingine, akaiita Leo, akisema kwa kinywa cha Daudi baadaye sana, kwa maneno yaliyotangulia kunenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu.”
Againe he appointed in Dauid a certaine day, by To day, after so long a time, saying, as it is sayd, This day, if ye heare his voyce, harden not your hearts.
8 Kwa maana kama Yoshua alikuwa amewapa raha, Mungu hangesema tena baadaye kuhusu siku nyingine.
For if Iesus had giuen them rest, then would he not after this haue spoke of an other day.
9 Kwa hiyo basi, imebaki raha ya Sabato kwa ajili ya watu wa Mungu;
There remaineth therefore a rest to the people of God.
10 kwa kuwa kila mmoja aingiaye katika raha ya Mungu pia hupumzika kutoka kazi zake mwenyewe, kama vile Mungu alivyopumzika kutoka kazi zake.
For he that is entred into his rest, hath also ceased from his owne works, as God did from his.
11 Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha hiyo, ili kwamba asiwepo yeyote atakayeanguka kwa kufuata mfano wao wa kutokutii.
Let vs studie therefore to enter into that rest, lest any man fall after the same ensample of disobedience.
12 Kwa maana Neno la Mungu li hai tena lina nguvu. Lina makali kuliko upanga wowote wenye makali kuwili, hivyo linachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, viungo na mafuta yaliyo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
For the worde of God is liuely, and mightie in operation, and sharper then any two edged sword, and entreth through, euen vnto the diuiding asunder of the soule and the spirit, and of the ioints, and the marow, and is a discerner of the thoughtes, and the intents of the heart.
13 Wala hakuna kiumbe chochote kilichofichika machoni pa Mungu. Kila kitu kimefunuliwa na kiko wazi machoni pake yeye ambaye kwake ni lazima tutatoa hesabu.
Neither is there any creature, which is not manifest in his sight: but all things are naked and open vnto his eyes, with whome we haue to doe.
14 Kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu kuliko wote ambaye ameingia mbinguni, Yesu Mwana wa Mungu, basi na tushikamane sana kwa uthabiti na ule ukiri wa imani yetu.
Seeing then that wee haue a great hie Priest, which is entred into heauen, euen Iesus the Sonne of God, let vs holde fast our profession.
15 Kwa kuwa hatuna Kuhani Mkuu asiyeweza kuchukuliana na sisi katika udhaifu wetu, lakini tunaye mmoja ambaye alijaribiwa kwa kila namna, kama vile sisi tujaribiwavyo: lakini yeye hakutenda dhambi.
For we haue not an hie Priest, which can not be touched with the feeling of our infirmities, but was in all things tempted in like sort, yet without sinne.
16 Basi na tukikaribie kiti cha rehema kwa ujasiri, ili tupewe rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.
Let vs therefore goe boldly vnto ye throne of grace, that we may receiue mercy, and finde grace to helpe in time of neede.

< Wahebrania 4 >