< Wahebrania 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa bado ahadi ya kuingia rahani iko wazi, tujihadhari ili hata mmoja wenu asije akaikosa.
Lader os derfor, da der endnu staar en Forjættelse tilbage om at indgaa til hans Hvile, vogte os for, at nogen af eder skal mene, at han er kommen for silde.
2 Kwa maana sisi pia tumesikia Injili iliyohubiriwa kwetu, kama nao walivyosikia; lakini ujumbe ule waliousikia haukuwa na maana kwao, kwa sababu wale waliousikia hawakuuchanganya na imani.
Thi ogsaa os er der forkyndt godt Budskab ligesom hine; men Ordet, som de hørte, hjalp ikke dem, fordi det ikke var forenet med Troen hos dem, som hørte det.
3 Sasa sisi ambao tumeamini tunaingia katika ile raha, kama vile Mungu alivyosema, “Kwa hiyo nikaapa katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’” Lakini kazi yake ilikamilika tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
Thi vi gaa ind til Hvilen, vi, som ere komne til Troen, efter hvad han har sagt: „Saa svor jeg i min Vrede: Sandelig, de skulle ikke gaa ind til min Hvile,” omendskønt Gerningerne vare fuldbragte fra Verdens Grundlæggelse.
4 Kwa maana mahali fulani amezungumza kuhusu siku ya saba, akisema: “Katika siku ya saba Mungu alipumzika kutoka kazi zake zote.”
Thi han har et Sted sagt om den syvende Dag saaledes: „Og Gud hvilede paa den syvende Dag fra alle sine Gerninger.”
5 Tena hapo juu asema, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”
Og fremdeles paa dette Sted: „Sandelig, de skulle ikke gaa ind til min Hvile.”
6 Kwa hiyo inabaki kuwa wazi kwa wengine kuingia, nao wale wa kwanza waliopokea Injili walishindwa kuingia kwa sababu ya kutokutii.
Efterdi der altsaa staar tilbage, at nogle skulle gaa ind til den, og de, hvem der først blev forkyndt godt Budskab, ikke gik ind for deres Genstridigheds Skyld:
7 Kwa hiyo Mungu ameweka siku nyingine, akaiita Leo, akisema kwa kinywa cha Daudi baadaye sana, kwa maneno yaliyotangulia kunenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu.”
Saa bestemmer han atter en Dag: „I Dag,” siger han ved David lang Tid efter, (som ovenfor sagt): „I Dag, naar I høre hans Røst, da forhærder ikke eders Hjerter!”
8 Kwa maana kama Yoshua alikuwa amewapa raha, Mungu hangesema tena baadaye kuhusu siku nyingine.
Thi dersom Josva havde skaffet dem Hvile, da Vilde han ikke tale om en anden Dag siden efter.
9 Kwa hiyo basi, imebaki raha ya Sabato kwa ajili ya watu wa Mungu;
Altsaa er der en Sabbatshvile tilbage for Guds Folk.
10 kwa kuwa kila mmoja aingiaye katika raha ya Mungu pia hupumzika kutoka kazi zake mwenyewe, kama vile Mungu alivyopumzika kutoka kazi zake.
Thi den, som er gaaet ind til hans Hvile, Ogsaa han har faaet Hvile fra sine Gerninger, ligesom Gud fra sine.
11 Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha hiyo, ili kwamba asiwepo yeyote atakayeanguka kwa kufuata mfano wao wa kutokutii.
Lader os derfor gøre os Flid for at gaa ind til hin Hvile, for at ikke nogen skal falde ved den samme Genstridighed, som hine gave Eksempel paa.
12 Kwa maana Neno la Mungu li hai tena lina nguvu. Lina makali kuliko upanga wowote wenye makali kuwili, hivyo linachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, viungo na mafuta yaliyo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Thi Guds Ord er levende og kraftigt og skarpere end noget tveægget Sværd og trænger igennem, indtil det deler Sjæl og Aand, Ledemod saavel som Marv, og dømmer over Hjertets Tanker og Raad.
13 Wala hakuna kiumbe chochote kilichofichika machoni pa Mungu. Kila kitu kimefunuliwa na kiko wazi machoni pake yeye ambaye kwake ni lazima tutatoa hesabu.
Og ingen Skabning er usynlig for hans Aasyn; men alle Ting ere nøgne og udspændte for hans Øjne, hvem vi staa til Regnskab.
14 Kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu kuliko wote ambaye ameingia mbinguni, Yesu Mwana wa Mungu, basi na tushikamane sana kwa uthabiti na ule ukiri wa imani yetu.
Efterdi vi altsaa have en stor Ypperstepræst, som er gaaet igennem Himlene, Jesus, Guds Søn, da lader os holde fast ved Bekendelsen!
15 Kwa kuwa hatuna Kuhani Mkuu asiyeweza kuchukuliana na sisi katika udhaifu wetu, lakini tunaye mmoja ambaye alijaribiwa kwa kila namna, kama vile sisi tujaribiwavyo: lakini yeye hakutenda dhambi.
Thi vi have ikke en Ypperstepræst, som ej kan have Medlidenhed med vore Skrøbeligheder, men en saadan, som er fristet i alle Ting i Lighed med os, dog uden Synd.
16 Basi na tukikaribie kiti cha rehema kwa ujasiri, ili tupewe rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.
Derfor lader os træde frem med Frimodighed for Naadens Trone, for at vi kunne faa Barmhjertighed og finde Naade til betimelig Hjælp.

< Wahebrania 4 >