< Wahebrania 3 >

1 Kwa hiyo ndugu watakatifu, mnaoshiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
Vous donc, mes frères saints, participants à la vocation céleste, considérez l’apôtre et le pontife de notre confession, Jésus,
2 Alikuwa mwaminifu kwa yeye aliyemweka, kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
Qui est fidèle à celui qui l’a établi, comme Moïse lui-même l’a été dans toute sa maison.
3 Yesu ameonekana anastahili heshima kubwa kuliko Mose, kama vile mjenzi wa nyumba alivyo wa heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
Car lui a été jugé digne d’une gloire aussi élevée au-dessus de celle de Moïse, que l’est l’honneur du constructeur par rapport à la maison qu’il a bâtie.
4 Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini Mungu ni mjenzi wa kila kitu.
En effet, toute maison est bâtie par quelqu’un: or celui qui a créé toutes choses, c’est Dieu.
5 Basi Mose kama mtumishi alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, akishuhudia kwa yale ambayo yangetamkwa baadaye.
Moïse, à la vérité, a été fidèle dans toute la maison de Dieu, comme serviteur, pour rendre témoignage de tout ce qu’il devait dire;
6 Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana katika nyumba ya Mungu. Sisi ndio nyumba yake, kama tutashikilia sana ujasiri wetu na tumaini tunalojivunia.
Mais le Christ est comme fils dans sa maison; et cette maison c’est nous, si nous conservons fermement jusqu’à la fin la confiance et la gloire de l’espérance.
7 Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo: “Leo, kama mkiisikia sauti yake,
C’est pourquoi, selon ce que dit l’Esprit-Saint: Aujourd’hui, si vous entendez sa voix,
8 msiifanye mioyo yenu migumu, kama mlivyofanya katika uasi, wakati ule wa kujaribiwa jangwani,
N’endurcissez pas vos cœurs, comme dans l’irritation au jour de la tentation dans le désert,
9 ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima ingawa kwa miaka arobaini walikuwa wameyaona matendo yangu.
Où vos pères me tentèrent, m’éprouvèrent, et virent mes œuvres
10 Hiyo ndiyo sababu nilikasirikia kizazi kile, nami nikasema, ‘Siku zote mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.’
Pendant quarante ans; aussi je me suis courroucé contre cette génération, et j’ai dit: Leur cœur s’égare toujours. Ils n’ont point connu mes voies:
11 Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’”
Ainsi, j’ai juré dans ma colère: Ils n’entreront point dans mon repos.
12 Ndugu zangu, angalieni, asiwepo miongoni mwenu mtu mwenye moyo mwovu usioamini, unaojitenga na Mungu aliye hai.
Prenez donc garde, mes frères, qu’il ne se trouve dans aucun de vous un cœur mauvais d’incrédulité, qui vous éloigne du Dieu vivant
13 Lakini mtiane moyo mtu na mwenzake kila siku, maadamu iitwapo Leo, ili asiwepo hata mmoja wenu mwenye kufanywa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
Mais exhortez-vous chaque jour les uns les autres, pendant ce qui est appelé Aujourd’hui, de peur que quelqu’un de vous ne s’endurcisse par la séduction du péché.
14 Kwa kuwa tumekuwa washiriki wa Kristo, kama tukishikamana tu kwa uthabiti na tumaini letu la kwanza hadi mwisho.
Car nous avons été faits participants du Christ, si cependant nous conservons inviolablement jusqu’à la fin ce commencement de son être.
15 Kama ilivyonenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya wakati wa kuasi.”
Ainsi, tant qu’on dit: Aujourd’hui, si vous entendez sa voix, n’endurcissez pas vos cœurs, comme en cette irritation-là.
16 Basi ni nani waliosikia lakini bado wakaasi? Je, si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Mose?
Car quelques-uns l’ayant entendue, irritèrent le Seigneur; mais ce ne fut pas tous ceux que Moïse avait fait sortir de l’Egypte.
17 Lakini ni nani aliowakasirikia miaka arobaini? Je, si wale waliofanya dhambi ambao miili yao ilianguka jangwani?
Or qui sont ceux contre lesquels il fut irrité pendant quarante ans? N’est-ce pas contre ceux qui péchèrent, et dont les corps furent abattus dans le désert?
18 Ni nani hao ambao Mungu aliapa kuwa kamwe hawataingia rahani mwake isipokuwa ni wale waliokataa kutii?
Et qui sont ceux auxquels il jura qu’ils n’entreraient pas dans son repos, sinon ceux qui sont incrédules?
19 Hivyo tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Aussi voyons-nous qu’ils ne purent y entrer, à cause de leur incrédulité.

< Wahebrania 3 >