< Wahebrania 3 >
1 Kwa hiyo ndugu watakatifu, mnaoshiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
Wherefore, holy brethren, partakers of a heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our confession, [even] Jesus;
2 Alikuwa mwaminifu kwa yeye aliyemweka, kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
who was faithful to him that appointed him, as also was Moses in all his house.
3 Yesu ameonekana anastahili heshima kubwa kuliko Mose, kama vile mjenzi wa nyumba alivyo wa heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
For he hath been counted worthy of more glory than Moses, by so much as he that built the house hath more honour than the house.
4 Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini Mungu ni mjenzi wa kila kitu.
For every house is builded by some one; but he that built all things is God.
5 Basi Mose kama mtumishi alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, akishuhudia kwa yale ambayo yangetamkwa baadaye.
And Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were afterward to be spoken;
6 Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana katika nyumba ya Mungu. Sisi ndio nyumba yake, kama tutashikilia sana ujasiri wetu na tumaini tunalojivunia.
but Christ as a son, over his house; whose house are we, if we hold fast our boldness and the glorying of our hope firm unto the end.
7 Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo: “Leo, kama mkiisikia sauti yake,
Wherefore, even as the Holy Ghost saith, Today if ye shall hear his voice,
8 msiifanye mioyo yenu migumu, kama mlivyofanya katika uasi, wakati ule wa kujaribiwa jangwani,
Harden not your hearts, as in the provocation, Like as in the day of the temptation in the wilderness,
9 ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima ingawa kwa miaka arobaini walikuwa wameyaona matendo yangu.
Wherewith your fathers tempted [me] by proving [me], And saw my works forty years.
10 Hiyo ndiyo sababu nilikasirikia kizazi kile, nami nikasema, ‘Siku zote mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.’
Wherefore I was displeased with this generation, And said, They do alway err in their heart: But they did not know my ways;
11 Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’”
As I sware in my wrath, They shall not enter into my rest.
12 Ndugu zangu, angalieni, asiwepo miongoni mwenu mtu mwenye moyo mwovu usioamini, unaojitenga na Mungu aliye hai.
Take heed, brethren, lest haply there shall be in any one of you an evil heart of unbelief, in falling away from the living God:
13 Lakini mtiane moyo mtu na mwenzake kila siku, maadamu iitwapo Leo, ili asiwepo hata mmoja wenu mwenye kufanywa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
but exhort one another day by day, so long as it is called Today; lest any one of you be hardened by the deceitfulness of sin:
14 Kwa kuwa tumekuwa washiriki wa Kristo, kama tukishikamana tu kwa uthabiti na tumaini letu la kwanza hadi mwisho.
for we are become partakers of Christ, if we hold fast the beginning of our confidence firm unto the end:
15 Kama ilivyonenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya wakati wa kuasi.”
while it is said, Today if ye shall hear his voice, Harden not your hearts, as in the provocation.
16 Basi ni nani waliosikia lakini bado wakaasi? Je, si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Mose?
For who, when they heard, did provoke? nay, did not all they that came out of Egypt by Moses?
17 Lakini ni nani aliowakasirikia miaka arobaini? Je, si wale waliofanya dhambi ambao miili yao ilianguka jangwani?
And with whom was he displeased forty years? was it not with them that sinned, whose carcases fell in the wilderness?
18 Ni nani hao ambao Mungu aliapa kuwa kamwe hawataingia rahani mwake isipokuwa ni wale waliokataa kutii?
And to whom sware he that they should not enter into his rest, but to them that were disobedient?
19 Hivyo tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.
And we see that they were not able to enter in because of unbelief.