< Wahebrania 3 >

1 Kwa hiyo ndugu watakatifu, mnaoshiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
Wherefore, holy brethren, partakers of the heavenly vocation, consider the apostle and high priest of our confession, Jesus:
2 Alikuwa mwaminifu kwa yeye aliyemweka, kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
Who is faithful to him that made him, as was also Moses in all his house.
3 Yesu ameonekana anastahili heshima kubwa kuliko Mose, kama vile mjenzi wa nyumba alivyo wa heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
For this man was counted worthy of greater glory than Moses, by so much as he that hath built the house, hath greater honour than the house.
4 Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini Mungu ni mjenzi wa kila kitu.
For every house is built by some man: but he that created all things, is God.
5 Basi Mose kama mtumishi alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, akishuhudia kwa yale ambayo yangetamkwa baadaye.
And Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were to be said:
6 Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana katika nyumba ya Mungu. Sisi ndio nyumba yake, kama tutashikilia sana ujasiri wetu na tumaini tunalojivunia.
But Christ as the Son in his own house: which house are we, if we hold fast the confidence and glory of hope unto the end.
7 Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo: “Leo, kama mkiisikia sauti yake,
Wherefore, as the Holy Ghost saith: Today if you shall hear his voice,
8 msiifanye mioyo yenu migumu, kama mlivyofanya katika uasi, wakati ule wa kujaribiwa jangwani,
Harden not your hearts, as in the provocation; in the day of temptation in the desert,
9 ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima ingawa kwa miaka arobaini walikuwa wameyaona matendo yangu.
Where your fathers tempted me, proved and saw my works,
10 Hiyo ndiyo sababu nilikasirikia kizazi kile, nami nikasema, ‘Siku zote mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.’
Forty years: for which cause I was offended with this generation, and I said: They always err in heart. And they have not known my ways,
11 Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’”
As I have sworn in my wrath: If they shall enter into my rest.
12 Ndugu zangu, angalieni, asiwepo miongoni mwenu mtu mwenye moyo mwovu usioamini, unaojitenga na Mungu aliye hai.
Take heed, brethren, lest perhaps there be in any of you an evil heart of unbelief, to depart from the living God.
13 Lakini mtiane moyo mtu na mwenzake kila siku, maadamu iitwapo Leo, ili asiwepo hata mmoja wenu mwenye kufanywa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
But exhort one another every day, whilst it is called today, that none of you be hardened through the deceitfulness of sin.
14 Kwa kuwa tumekuwa washiriki wa Kristo, kama tukishikamana tu kwa uthabiti na tumaini letu la kwanza hadi mwisho.
For we are made partakers of Christ: yet so, if we hold the beginning of his substance firm unto the end.
15 Kama ilivyonenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya wakati wa kuasi.”
While it is said, Today if you shall hear his voice, harden not your hearts, as in that provocation.
16 Basi ni nani waliosikia lakini bado wakaasi? Je, si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Mose?
For some who heard did provoke: but not all that came out of Egypt by Moses.
17 Lakini ni nani aliowakasirikia miaka arobaini? Je, si wale waliofanya dhambi ambao miili yao ilianguka jangwani?
And with whom was he offended forty years? Was it not with them that sinned, whose carcasses were overthrown in the desert?
18 Ni nani hao ambao Mungu aliapa kuwa kamwe hawataingia rahani mwake isipokuwa ni wale waliokataa kutii?
And to whom did he swear, that they should not enter into his rest: but to them that were incredulous?
19 Hivyo tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.
And we see that they could not enter in, because of unbelief.

< Wahebrania 3 >