< Wahebrania 2 >
1 Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha.
Por lo tanto, debemos prestar más atención a las cosas que se escucharon, para que no nos desviemos.
2 Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki,
Porque si la palabra hablada por medio de los ángeles resultó firme, y toda transgresión y desobediencia recibió un justo castigo,
3 je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia.
¿cómo escaparemos nosotros si descuidamos una salvación tan grande, la cual, habiendo sido hablada al principio por medio del Señor, nos fue confirmada por los que oyeron,
4 Pia Mungu aliushuhudia kwa ishara, maajabu na kwa miujiza mbalimbali, na karama za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake.
testificando Dios también con ellos, tanto por señales como por prodigios, por diversas obras de poder y por dones del Espíritu Santo, según su propia voluntad?
5 Mungu hakuuweka ulimwengu ujao ambao tunanena habari zake chini ya malaika.
Porque no sometió a los ángeles el mundo venidero, del que hablamos.
6 Lakini kuna mahali mtu fulani ameshuhudia akisema: “Mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
Pero uno ha testificado en alguna parte, diciendo, “¿Qué es el hombre, para que pienses en él? ¿O el hijo del hombre, que se preocupa por él?
7 Umemfanya chini kidogo kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
Lo hiciste un poco más bajo que los ángeles. Lo coronaste de gloria y honor.
8 nawe umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Kwa kuweka vitu vyote chini yake, Mungu hakuacha kitu chochote ambacho hakukiweka chini ya mwanadamu. Lakini kwa sasa, hatuoni kwamba kila kitu kiko chini yake.
Has sometido todas las cosas bajo sus pies”. Porque al someter todas las cosas a él, no dejó nada que no le estuviera sometido. Pero ahora todavía no vemos todas las cosas sometidas a él.
9 Lakini twamwona Yesu, aliyefanywa chini kidogo kuliko malaika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu alistahimili mauti, ili kwamba kwa neema ya Mungu apate kuonja mauti kwa ajili ya kila mtu.
Pero vemos al que ha sido hecho un poco más bajo que los ángeles, Jesús, a causa del sufrimiento de la muerte, coronado de gloria y honor, para que por la gracia de Dios probara la muerte por todos.
10 Ili kuwaleta wana wengi katika utukufu, ilifaa kwamba Mungu, ambaye ni kwa ajili yake na kupitia kwake kila kitu kimekuwepo, amkamilishe mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso.
Porque convenía a aquel por quien son todas las cosas y por quien son todas las cosas, al llevar a muchos niños a la gloria, perfeccionar por aflicciones al autor de la salvación de ellos.
11 Yeye awafanyaye watu kuwa watakatifu, pamoja na hao ambao hufanywa watakatifu, wote hutoka katika jamaa moja. Hivyo Yesu haoni aibu kuwaita ndugu zake.
Porque tanto el que santifica como los santificados proceden todos de uno, por lo que no se avergüenza de llamarlos hermanos,
12 Yeye husema, “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; mbele ya kusanyiko nitaimba sifa zako.”
diciendo, “Declararé tu nombre a mis hermanos. Entre la congregación cantaré tu alabanza”.
13 Tena, “Nitaweka tumaini langu kwake.” Tena anasema, “Niko hapa, pamoja na watoto ambao Mungu amenipa.”
De nuevo: “Pondré mi confianza en él”. De nuevo: “He aquí que estoy con los hijos que Dios me ha dado”.
14 Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani ibilisi,
Puesto que los hijos participaron de la carne y de la sangre, también él participó de lo mismo, para anular por medio de la muerte al que tenía el poder de la muerte, es decir, al diablo,
15 na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti.
y liberar a todos los que, por temor a la muerte, estaban durante toda su vida sujetos a esclavitud.
16 Kwa kuwa ni dhahiri kwamba hakuja kusaidia malaika, bali uzao wa Abrahamu.
Porque ciertamente, no da ayuda a los ángeles, sino que da ayuda a la descendencia de Abraham.
17 Kwa sababu hii ilibidi afanane na ndugu zake kwa kila hali, ili apate kuwa Kuhani Mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika kumtumikia Mungu, ili pia apate kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za watu.
Por eso estaba obligado en todo a hacerse semejante a sus hermanos, para llegar a ser un sumo sacerdote misericordioso y fiel en las cosas de Dios, para expiar los pecados del pueblo.
18 Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.
Porque habiendo sufrido él mismo la tentación, puede ayudar a los que son tentados.