< Wahebrania 2 >

1 Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha.
ܡܛܠ ܗܢܐ ܚܝܒܝܢܢ ܕܝܬܝܪܐܝܬ ܢܗܘܐ ܙܗܝܪܝܢ ܒܡܕܡ ܕܫܡܥܢ ܕܠܐ ܢܦܠ
2 Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki,
ܐܢ ܓܝܪ ܡܠܬܐ ܕܐܬܡܠܠܬ ܒܝܕ ܡܠܐܟܐ ܐܫܬܪܪܬ ܘܟܠ ܕܫܡܥܗ ܘܥܒܪ ܥܠܝܗ ܩܒܠ ܦܘܪܥܢܐ ܒܟܐܢܘܬܐ
3 je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia.
ܐܝܟܢܐ ܚܢܢ ܢܥܪܘܩ ܐܢ ܢܒܤܐ ܥܠ ܐܝܠܝܢ ܕܗܢܘܢ ܐܢܘܢ ܚܝܝܢ ܗܢܘܢ ܕܫܪܝܘ ܡܢ ܡܪܢ ܠܡܬܡܠܠܘ ܘܡܢ ܐܝܠܝܢ ܕܡܢܗ ܫܡܥܘ ܒܢ ܐܫܬܪܪܘ
4 Pia Mungu aliushuhudia kwa ishara, maajabu na kwa miujiza mbalimbali, na karama za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake.
ܟܕ ܤܗܕ ܥܠܝܗܘܢ ܐܠܗܐ ܒܐܬܘܬܐ ܘܒܬܕܡܪܬܐ ܘܒܚܝܠܐ ܡܫܚܠܦܐ ܘܒܦܘܠܓܐ ܕܪܘܚܐ ܕܩܘܕܫܐ ܕܐܬܝܗܒܘ ܐܝܟ ܨܒܝܢܗ
5 Mungu hakuuweka ulimwengu ujao ambao tunanena habari zake chini ya malaika.
ܠܐ ܗܘܐ ܓܝܪ ܠܡܠܐܟܐ ܫܥܒܕ ܥܠܡܐ ܕܥܬܝܕ ܕܥܠܘܗܝ ܡܡܠܠܝܢܢ
6 Lakini kuna mahali mtu fulani ameshuhudia akisema: “Mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
ܐܠܐ ܐܝܟ ܕܡܤܗܕ ܟܬܒܐ ܘܐܡܪ ܡܢܘ ܓܒܪܐ ܕܥܗܕܬܝܗܝ ܘܒܪܗ ܕܐܢܫܐ ܕܤܥܪܬܝܗܝ
7 Umemfanya chini kidogo kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
ܐܡܟܬܝܗܝ ܩܠܝܠ ܡܢ ܡܠܐܟܐ ܬܫܒܘܚܬܐ ܘܐܝܩܪܐ ܤܡܬ ܒܪܝܫܗ ܘܐܫܠܛܬܝܗܝ ܒܥܒܕܐ ܕܐܝܕܝܟ
8 nawe umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Kwa kuweka vitu vyote chini yake, Mungu hakuacha kitu chochote ambacho hakukiweka chini ya mwanadamu. Lakini kwa sasa, hatuoni kwamba kila kitu kiko chini yake.
ܘܟܠ ܡܕܡ ܫܥܒܕܬ ܬܚܝܬ ܪܓܠܘܗܝ ܒܗܝ ܕܝܢ ܕܟܠ ܡܕܡ ܫܥܒܕ ܠܗ ܠܐ ܫܒܩ ܡܕܡ ܕܠܐ ܡܫܥܒܕ ܗܫܐ ܕܝܢ ܠܐ ܥܕܟܝܠ ܚܙܝܢܢ ܕܟܠ ܡܕܡ ܡܫܥܒܕ ܠܗ
9 Lakini twamwona Yesu, aliyefanywa chini kidogo kuliko malaika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu alistahimili mauti, ili kwamba kwa neema ya Mungu apate kuonja mauti kwa ajili ya kila mtu.
ܗܘ ܕܝܢ ܕܡܟ ܩܠܝܠ ܡܢ ܡܠܐܟܐ ܚܙܝܢܢ ܕܗܘܝܘ ܝܫܘܥ ܡܛܠ ܚܫܐ ܕܡܘܬܗ ܘܬܫܒܘܚܬܐ ܘܐܝܩܪܐ ܤܝܡ ܒܪܝܫܗ ܗܘ ܓܝܪ ܒܛܝܒܘܬܗ ܐܠܗܐ ܚܠܦ ܟܠܢܫ ܛܥܡ ܡܘܬܐ
10 Ili kuwaleta wana wengi katika utukufu, ilifaa kwamba Mungu, ambaye ni kwa ajili yake na kupitia kwake kila kitu kimekuwepo, amkamilishe mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso.
ܝܐܐ ܗܘܐ ܓܝܪ ܠܗܘ ܕܟܠ ܒܐܝܕܗ ܘܟܠ ܡܛܠܬܗ ܘܒܢܝܐ ܤܓܝܐܐ ܐܥܠ ܠܬܫܒܘܚܬܐ ܕܠܪܝܫܐ ܕܚܝܝܗܘܢ ܒܚܫܗ ܢܓܡܪܝܘܗܝ
11 Yeye awafanyaye watu kuwa watakatifu, pamoja na hao ambao hufanywa watakatifu, wote hutoka katika jamaa moja. Hivyo Yesu haoni aibu kuwaita ndugu zake.
ܗܘ ܓܝܪ ܕܩܕܫ ܘܗܢܘܢ ܕܐܬܩܕܫܘ ܡܢ ܚܕ ܐܢܘܢ ܟܠܗܘܢ ܡܛܠ ܗܢܐ ܠܐ ܒܗܬ ܕܢܩܪܐ ܐܢܘܢ ܐܚܘܗܝ
12 Yeye husema, “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; mbele ya kusanyiko nitaimba sifa zako.”
ܟܕ ܐܡܪ ܐܤܒܪ ܫܡܟ ܠܐܚܝ ܘܒܓܘܗ ܕܥܕܬܐ ܐܫܒܚܟ
13 Tena, “Nitaweka tumaini langu kwake.” Tena anasema, “Niko hapa, pamoja na watoto ambao Mungu amenipa.”
ܘܬܘܒ ܕܐܢܐ ܐܗܘܐ ܬܟܝܠ ܥܠܘܗܝ ܘܬܘܒ ܗܐ ܐܢܐ ܘܒܢܝܐ ܕܝܗܒ ܠܝ ܐܠܗܐ
14 Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani ibilisi,
ܡܛܠ ܓܝܪ ܕܒܢܝܐ ܐܫܬܘܬܦܘ ܒܒܤܪܐ ܘܕܡܐ ܐܦ ܗܘ ܒܗ ܒܕܡܘܬܐ ܐܫܬܘܬܦ ܒܗܝܢ ܒܗܠܝܢ ܕܒܡܘܬܗ ܢܒܛܠ ܠܡܢ ܕܐܚܝܕ ܫܘܠܛܢܐ ܕܡܘܬܐ ܕܐܝܬܘܗܝ ܤܛܢܐ
15 na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti.
ܘܢܫܪܐ ܠܗܢܘܢ ܐܝܠܝܢ ܕܒܕܚܠܬܐ ܕܡܘܬܐ ܒܟܠܗܘܢ ܚܝܝܗܘܢ ܡܫܥܒܕܝܢ ܗܘܘ ܠܥܒܕܘܬܐ
16 Kwa kuwa ni dhahiri kwamba hakuja kusaidia malaika, bali uzao wa Abrahamu.
ܠܐ ܗܘܐ ܓܝܪ ܥܠ ܡܠܐܟܐ ܡܫܠܛ ܗܘܐ ܡܘܬܐ ܐܠܐ ܥܠ ܙܪܥܗ ܕܐܒܪܗܡ ܡܫܠܛ ܗܘܐ
17 Kwa sababu hii ilibidi afanane na ndugu zake kwa kila hali, ili apate kuwa Kuhani Mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika kumtumikia Mungu, ili pia apate kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za watu.
ܡܛܠ ܗܢܐ ܙܕܩ ܗܘܐ ܕܒܟܠ ܡܕܡ ܢܬܕܡܐ ܠܐܚܘܗܝ ܕܢܗܘܐ ܡܪܚܡܢܐ ܘܪܒ ܟܘܡܪܐ ܡܗܝܡܢܐ ܒܕܐܠܗܐ ܘܢܗܘܐ ܡܚܤܐ ܥܠ ܚܛܗܘܗܝ ܕܥܡܐ
18 Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.
ܒܗܝ ܓܝܪ ܕܗܘ ܚܫ ܘܐܬܢܤܝ ܡܫܟܚ ܕܢܥܕܪ ܠܐܝܠܝܢ ܕܡܬܢܤܝܢ

< Wahebrania 2 >