< Wahebrania 13 >

1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
Blifver faste i broderlig kärlek.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
Förgäter icke att herberga; ty dermed hafva somliga fått Änglar, ovetandes, till herberges.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
Tänker på dem som bundne äro, såsom medbundne; och på dem som bedröfvelse lida, såsom de der ock af lekamenen äro.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
Ägtenskapet skall hållas ärligit ibland alla, och ägtenskapets säng obesmittad; men bolare och horkarlar skall Gud döma.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
Umgängelsen vare utan girighet; och låter eder nöja med det I hafven; ty han sade: Jag skall icke öfvergifva eller förlåta dig;
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
Så att vi dristeliga måga säga: Herren är min hjelpare, och jag vill icke frukta; hvad kan en menniska göra mig?
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
Tänker på edra lärare, de eder Guds ord sagt hafva, och efterföljer deras tro; skådande hvad ända deras umgängelse hade.
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
Jesus Christus i går och i dag, och han desslikes i evighet. (aiōn g165)
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
Låter eder icke omföras med mångahanda och främmande lärdom; ty det är godt att stadfästa hjertat med nådene; icke med maten; hvilken intet gagnat hafver dem, som dermed umgått hafva.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
Vi hafve ett altare, af hvilko de hafva icke magt att äta, som tjena i tabernaklet.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
Ty ehvad djurs blod, som öfverste Presten, för syndene, inbär uti det heliga, deras kroppar uppbrännas utom lägret.
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
Derföre ock Jesus, på det han skulle helga folket med sitt eget blod, hafver han lidit utom porten.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
Så låt oss nu gå ut till honom utu lägret, och bära hans smälek.
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
Ty vi hafve här ingen varaktig stad, utan vi sökom efter den tillkommande.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Så låt oss nu genom honom alltid offra Gudi lofoffer, det är, läpparnas frukt, de hans Namn bekänna.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
Förgäter icke göra väl, och meddela; ty sådana offer täckas Gudi.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
Varer edra lärare lydige, och följer dem; ty de vaka öfver edra själar, såsom de der räkenskap göra skola; på det de måga det göra med fröjd, och icke med suckan; ty det är eder icke nyttigt.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
Beder för oss; vår tröst är den att vi ett godt samvet hafve, och vinnlägge oss hafva en god umgängelse när alla;
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
Men aldramest beder jag eder, att I sådant gören, att jag med det snaresta måtte komma till eder.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
Men fridsens Gud, som igenfört hafver ifrå de döda den stora Fåraherdan, genom dess eviga Testamentsens blod, vår Herra Jesum; (aiōnios g166)
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Han göre eder skickeliga uti allt godt verk, till att göra sin vilja, och skaffe uti eder hvad honom täckeligit är, genom Jesum Christum; hvilken vare ära af evighet i evighet. Amen. (aiōn g165)
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
Jag förmanar eder, käre bröder, tager förmanelsens ord till godo; ty jag hafver eder med få ord tillskrifvit.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
Veter, att brodren Timotheus lös är; med hvilkom, om han snart kommer, vill jag se eder.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
Helser alla edra lärare, och all helgon. Eder helsa bröderne uti Valland.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Nåd vare med eder allom. Amen.

< Wahebrania 13 >