< Wahebrania 13 >

1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
Permaneça a caridade fraternal.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
Não vos esqueçais da hospitalidade, porque por ela alguns, não o sabendo, hospedaram anjos.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
Lembrai-vos dos presos, como se juntamente estivesseis presos, e dos maltratados, como o sendo vós mesmos também no corpo.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
Venerado seja entre todos o matrimônio e a cama sem mácula; porém aos fornicadores e adúlteros Deus os julgará.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
Sejam os vossos costumes sem avareza, contentando-vos com o presente; porque ele disse: Não te deixarei, nem te desampararei.
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
De maneira que com confiança ousemos dizer: O Senhor é o meu ajudador, e não temerei o que o homem me possa fazer.
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
Lembrai-vos dos vossos pastores, que vos falaram a palavra de Deus, a fé dos quais imitai, atentando para a maneira da vida deles.
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
Jesus Cristo é o mesmo ontem, e hoje, e eternamente. (aiōn g165)
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
Não vos deixeis levar ao redor por doutrinas várias e estranhas, porque bom é que o coração se fortifique com graça, e não com manjares, os quais de nada aproveitaram aos que a eles se entregaram.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
Temos um altar, do qual não tem poder de comer os que servem ao tabernáculo.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
Porque os corpos dos animais, cujo sangue é, pelo pecado, trazido pelo sumo sacerdote para o santuário, são queimados fora do arraial.
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
Portanto também Jesus, para santificar o povo pelo seu próprio sangue, padeceu fora da porta.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
Saiamos pois a ele fora do arraial, levando o seu vitupério.
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
Porque não temos aqui cidade permanente, mas buscamos a futura.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Portanto ofereçamos sempre por ele a Deus sacrifício de louvor, isto é, o fruto dos lábios que confessam o seu nome.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
E não vos esqueçais da beneficência e comunicação, porque com tais sacrifícios Deus se agrada.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
Obedecei a vossos pastores, e sujeitai-vos a eles; porque velam por vossas almas, como aqueles que hão de dar conta delas; para que o façam com alegria e não gemendo; porque isso não vos seria útil.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
Rogai por nós, porque confiamos que temos boa consciência, como aqueles que em tudo querem portar-se honestamente.
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
E rogo-vos com instância que assim o façais, para que eu mais depressa vos seja restituído.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
Ora o Deus de paz, que pelo sangue do concerto eterno tornou a trazer dos mortos a nosso Senhor Jesus Cristo, grande pastor das ovelhas, (aiōnios g166)
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Vos aperfeiçoe em toda a boa obra, para fazerdes a sua vontade, obrando em vós o que perante ele é agradável por Cristo Jesus, ao qual seja glória para todo o sempre. amém. (aiōn g165)
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
Rogo-vos, porém, irmãos, que suporteis a palavra desta exortação; porque abreviadamente vos escrevi.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
Sabei que já está solto o irmão Timotheo, com o qual (se vier depressa) vos verei.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
Saudai a todos os vossos chefes e a todos os santos. Os de Itália vos saudam.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
A graça seja com todos vós. amém.

< Wahebrania 13 >