< Wahebrania 13 >

1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
Que la charité fraternelle demeure en vous:
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
Et ne négligez pas l’hospitalité, car c’est par elle que quelques-uns ont donné, sans le savoir, l’hospitalité à des anges.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
Souvenez-vous de ceux qui sont dans les liens, comme si vous y étiez avec eux; et des affligés, comme demeurant vous-mêmes dans un corps.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
Que le mariage soit honoré en toutes choses, et le lit nuptial sans souillure; car les fornicateurs et les adultères. Dieu les jugera.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
Que votre vie soit sans avarice, vous contentant de ce que vous avez; car lui-même a dit: Je ne t’abandonnerai ni ne te délaisserai.
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
Ainsi, disons avec confiance: Le Seigneur m’est aide; je ne craindrai point ce qu’un homme peut me faire.
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
Souvenez-vous de vos préposés qui vous ont prêché la parole de Dieu; et considérant la fin de leur vie, imitez leur foi.
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
Jésus-Christ était hier, il est aujourd’hui, et il sera le même dans tous les siècles. (aiōn g165)
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
Ne vous laissez point emporter à des doctrines diverses et étrangères. Car il est bon d’affermir le cœur par la grâce, et non par des distinctions de viandes, lesquelles n’ont point servi à ceux qui s’y conformaient.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
Nous avons un autel dont n’ont pas le droit de manger ceux qui servent dans le tabernacle.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
Car les corps des animaux dont le sang est porté par le pontife dans le sanctuaire sont brûlés hors du camp.
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
C’est pourquoi Jésus lui-même, pour sanctifier le peuple par son sang, a souffert hors de la porte.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
Allons donc à lui hors du camp, portant son opprobre.
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
Car nous n’avons point ici de cité permanente, mais nous cherchons la cité future.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Par lui donc offrons à Dieu une hostie de louange, c’est-à-dire le fruit de lèvres qui confessent son nom.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
N’oubliez point non plus la charité et la communication de vos biens; car c’est par de telles hosties qu’on se concilie Dieu.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
Obéissez à vos préposés, et soyez-leur soumis (car ce sont eux qui veillent, comme devant rendre compte de vos âmes), afin qu’ils le fassent avec joie, et non en gémissant; cela ne vous serait pas avantageux.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
Priez pour nous; car nous croyons avoir une bonne conscience, voulant en toutes choses nous bien conduire.
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
Et je vous conjure, avec une nouvelle instance, de le faire, afin que je vous sois plus tôt rendu.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
Que le Dieu de paix, qui, par le sang du testament éternel, a retiré d’entre les morts le grand pasteur des brebis, Notre-Seigneur Jésus-Christ, (aiōnios g166)
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Vous rende propres à tout bien, afin que vous fassiez sa volonté; lui-même faisant eu vous ce qui lui est agréable, par Jésus-Christ à qui est la gloire dans les siècle des siècles. Amen. (aiōn g165)
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
Je vous prie, mes frères, d’agréer cette parole de consolation, car je ne vous ai écrit qu’en peu de mots.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
Sachez que notre frère Timothée est en liberté; c’est avec lui (s’il vient bientôt) que je vous verrai.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
Saluez tous vos préposés et tous les saints. Les frères d’Italie vous saluent.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Que la grâce soit avec vous tous. Amen.

< Wahebrania 13 >