< Wahebrania 13 >

1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
Let brotherly love continue.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
Be not forgetful of hospitality; for thereby some have entertained angels, not knowing it.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
Remember those that are in bonds, as if bound with them: and those that suffer evil as being yourselves also in the body.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
Marriage is honorable in all, and the bed is not defiled: but whoremongers and adulterers God will judge.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
Let your conversation be free from covetousness, and be contented with what ye have: for He hath said, I will not leave thee; I will never, never forsake thee.
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
So that we may say with courage, The Lord is my helper, and I will not fear what man shall do unto me.
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
Remember your guides, who spake the word of God to you; whose faith imitate, considering the happy end of their conversation.
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
Jesus Christ is the same yesterday, to day, and for ever: (aiōn g165)
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
be not then carried about by various and strange doctrines; for it is good that the heart be established by grace, and not in meats, in which those that have been most exact, have not profited by them.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
We have an altar, of which those who perform service in the tabernacle have no right to eat.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
As the bodies of those animals, whose blood being offered for sin is brought into the holy place by the high-priest, are not eaten, but are burnt without the camp.
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
Wherefore Jesus also, that He might sanctify the people by his own blood, suffered without the gate.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
Let us then go out unto Him without the camp, bearing his reproach: for we have here no continuing city,
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
but are seeking that which is to come.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
By him therefore let us offer the sacrifice of praise to God continually, that is, the fruit of our lips giving thanks to his name.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
But to do good and to communicate forget not; for with such sacrifices God is well pleased.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
Be ruled by those that are your guides, and submit to them: for they watch for your souls; (as those that must give an account) that they may do it with joy and not with uneasiness: for this were unprofitable for you.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
Pray for us; for we are confident that we have a good conscience, desiring in all things to behave well.
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
And I the more earnestly intreat you to do this, that I may be restored to you the sooner.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
Now the God of peace, who brought again from the dead our Lord Jesus, the great shepherd of the sheep, by the blood of the everlasting covenant, (aiōnios g166)
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
make you perfect in every good work, to do his will, working in you that which is well-pleasing in his sight, through Jesus Christ; to whom be glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
I beseech you, brethren, bear with this word of exhortation: as I have written to you in brief.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
Know that our brother Timothy is set at liberty, with whom (if he come soon) I will see you.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
Salute all that preside over you, yea and all the saints. They of Italy salute you.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Grace be with you all. Amen.

< Wahebrania 13 >