< Wahebrania 13 >
1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
Brotherly love should abide.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
Of hospitality not do forget; through this for unawares some have entertained angels.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
do remember prisoners as bound with [them], [and] those being mistreated as also yourselves being in [the] body.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
Honorable [let] marriage [be] in all and the marriage bed undefiled; [the] sexually immoral (for *N(k)O*) and adulterers will judge God.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
[Let be] without covetousness [your] manner of life; being satisfied with the present; He Himself for has said: Certainly not you shall I leave, nor certainly not you (shall I forsake; *NK(o)*)
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
So are confident we to say: [The] Lord [is] my helper, and not I will be afraid; what will do to me man?
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
do remember those leading you, who spoke to you the word of the God, of whom considering the outcome of [their] way of life, do imitate the faith.
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn )
Jesus Christ yesterday and today [is] the same and to the ages. (aiōn )
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
by teachings various and strange not (do be taken away; *N(k)O*) [it is] good for by grace to be strengthened for the heart not by foods in which not they profited those (being devoted. *N(k)O*)
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
We have an altar from which to eat not they have authority those in the tabernacle serving.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
Whose for is brought of animals the blood [as sacrifices] for sin into the Holy [Places] through the high priest, of those the bodies are burned outside the camp.
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
Therefore also Jesus, so that he may sanctify through the own blood the people, outside the gate suffered.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
Therefore we may go forth to Him outside the camp the reproach of Him bearing;
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
Not for we have here an abiding city, but the coming [one] we are seeking for.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Through Him then we may offer [the] sacrifice of praise (through *N(K)O*) (all [times] *N(k)O*) to God, That is [the] fruit of [the] lips confessing the name of Him.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
And the good and of sharing not do be forgetful; with such for sacrifices is well pleased God.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
do obey to those leading you and do be submissive; they themselves for watch over the souls of you as an account to be giving that with joy this they may do and not groaning; unprofitable indeed for you [is] this.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
do pray for us; (we are assured *N(k)O*) for that a good conscience we have in all things well desiring to conduct ourselves.
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
More abundantly now I exhort [you] this to do, so that quicker I may be restored to you.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios )
[May] the now God of peace, having brought out from [the] dead the Shepherd of the sheep great by [the] blood of [the] covenant eternal, the Lord of us Jesus, (aiōnios )
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
would he equip you in everything (work *KO*) good in order to do the will of Him working in (us *N(K)O*) that which [is] well pleasing before Him through Jesus Christ; to whom [be] the glory to the ages of the ages, Amen. (aiōn )
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
I exhort now you, brothers, do bear with the word of exhortation; only for in few words I have written to you.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
You know the brother (of us *no*) Timothy released with whom if quicker he shall come, I will see you.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
do greet all those leading you and all the saints. Greet you those from Italy.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Grace [be] with all of you. (Amen. *KO*) (to Hebrews it was written from Italy through Timothy. *K*)