< Wahebrania 13 >

1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
Let brotherly love continue.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
Do not forget hospitality to strangers, for in doing so some have entertained angels without knowing it.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
Remember the prisoners as if chained with them, those who are being mistreated as if you yourselves were physically there.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
Marriage is honorable among all and the marriage bed undefiled, but God will judge fornicators and adulterers.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
Your way of life should be free from the love of money, being content with what you have, because He Himself has said: “I absolutely will not desert you; I most certainly will not abandon you.”
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
So we can say with confidence: “The Lord is my helper; I will not fear. What can man do to me?”
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
Remember your leaders, those who spoke the Word of God to you, whose faith imitate, considering the outcome of their conduct.
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
Jesus Christ is Himself, yesterday and today and into the ages. (aiōn g165)
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
Do not be carried away by various and strange teachings, because it is good that the heart be established by grace, not foods, by which those who were so occupied were not benefited.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
We have an altar from which those who serve in the Tabernacle have no right to eat.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
Because the bodies of the animals—whose blood, concerning sin, is brought into the Holies by the high priest—are burned up outside the camp,
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
therefore Jesus also, so that He might sanctify the people by His own blood, suffered outside the city gate.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
So then, let us go out to Him, outside the camp, bearing His disgrace;
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
because here we do not have a permanent city, but we seek the coming one.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Through Him therefore, at all times, let us offer up a sacrifice of praise to God—the fruit of lips that identify with His name.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
(But do not forget to do good and to share, for with such sacrifices God is pleased.)
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
Obey your leaders and submit, for they keep watch over your souls, as those who must give account, so that they may do it with joy and not sighing (which would be unprofitable for you).
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
Pray for us; for we are confident that we have a good conscience, desiring to live commendably in all things;
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
I especially urge you to do this so that I may be restored to you more quickly.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
Now may the God of peace—who through the blood of the eternal covenant brought back from the dead our Lord Jesus, that great Shepherd of the sheep— (aiōnios g166)
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
equip you for every good work to do His will, working in you what is well pleasing in His sight, through Jesus Christ, to whom be the glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
Now I appeal to you, brothers, bear with this word of exhortation, for I have written to you in few words.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
Know that brother Timothy has been released, with whom I will see you, if he comes quickly.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
Greet all your leaders and all the saints. Those from Italy greet you.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
The Grace be with you all. Amen.

< Wahebrania 13 >