< Wahebrania 13 >

1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
May fraternal charity remain in you.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
And do not be willing to forget hospitality. For by it, certain persons, without realizing it, have received Angels as guests.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
Remember those who are prisoners, just as if you were imprisoned with them, and those who endure hardships, just as if you were in their place.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
May marriage be honorable in every way, and may the marriage bed be immaculate. For God will judge fornicators and adulterers.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
Let your behavior be without avarice; be content with what you are offered. For he himself has said, “I will not abandon you, and I will not neglect you.”
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
So then, we may confidently say, “The Lord is my helper. I will not fear what man can do to me.”
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
Remember your leaders, who have spoken the Word of God to you, whose faith you imitate, by observing the goal of their way of life:
8 Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
Jesus Christ, yesterday and today; Jesus Christ forever. (aiōn g165)
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
Do not be led away by changing or strange doctrines. And it is best for the heart to be sustained by grace, not by foods. For the latter have not been as useful to those who walked by them.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
We have an altar: those who serve in the tabernacle have no authority to eat from it.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
For the bodies of those animals whose blood is carried into the Holy of holies by the high priest, on behalf of sin, are burned outside the camp.
12 Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
Because of this, Jesus, too, in order to sanctify the people by his own blood, suffered outside the gate.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
And so, let us go forth to him, outside the camp, bearing his reproach.
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
For in this place, we have no everlasting city; instead, we seek one in the future.
15 Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Therefore, through him, let us offer the sacrifice of continual praise to God, which is the fruit of lips confessing his name.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
But do not be willing to forget good works and fellowship. For God is deserving of such sacrifices.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
Obey your leaders and be subject to them. For they watch over you, as if to render an account of your souls. So then, may they do this with joy, and not with grief. Otherwise, it would not be as helpful to you.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
Pray for us. For we trust that we have a good conscience, being willing to conduct ourselves well in all things.
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
And I beg you, all the more, to do this, so that I may be quickly returned to you.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
Then may the God of peace, who led back from the dead that great Pastor of sheep, our Lord Jesus Christ, with the blood of the eternal testament, (aiōnios g166)
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
equip you with all goodness, so that you may do his will. May he accomplish in you whatever is pleasing in his sight, through Jesus Christ, to whom is glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
And I beg you, brothers, that you may permit this word of consolation, especially since I have written to you with few words.
23 Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
Know that our brother Timothy has been set free. If he arrives soon, then I will see you with him.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
Greet all your leaders and all the saints. The brothers from Italy greet you.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Grace be with you all. Amen.

< Wahebrania 13 >