< Wahebrania 11 >

1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
Vera pa je trdno pričakovanje tistega, kar se upa, dokaz stvarî, katere se ne vidijo.
2 Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
V tej namreč so starejši pričanje prejeli.
3 Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn g165)
Po veri umemo, da so svetovi osnovani bili po besedi Božji, tako da ni iz prikazujočega se postalo, kar je vidno. (aiōn g165)
4 Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu bora zaidi kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
Po veri je daroval Abelj Bogu boljšo žrtev mimo Kajna, po kateri je bil izpričan za pravičnega, ker je Bog sam pričal po darovih, in po njej se še o mrtvem govori.
5 Kwa imani Enoki alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
Po veri je bil Enoh umaknen, da ni videl smrti "in ni ga bilo najti, ker ga je bil Bog umaknil." Kajti pred umaknenjem svojim dobil je pričanje, "da je Bogu po volji."
6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.
Brez vere pa je nemogoče biti po volji; kajti verovati je treba njemu, kateri se bliža Bogu, da je in da postane plačevalec njim, ki ga iščejo.
7 Kwa imani, Noa alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
Po veri je napravil Noe, na povelje, za to, kar se ni še videlo, v strahu Božjem skrinjo v rešenje hiše svoje; po njej je obsodil svet, in je postal dedič pravice po veri.
8 Kwa imani Abrahamu, alipoitwa aende mahali ambapo Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakokwenda.
Po veri je slušal Abraham poklican, naj izide v kraj, katerega je imel dobiti v dedščino, in izšel je ne vedoč, kam ide.
9 Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaki na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
Po veri je bival v deželi obljube kakor tuji, stanujoč v šatorih z Izakom in Jakobom sodedičema iste obljube.
10 Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
Kajti čakal je mesta imajočega podstave, katerega zidar in stvarnik je Bog.
11 Kwa imani Abrahamu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
Po veri je tudi sama Sara zadobila moč ustanoviti seme in rodila je, zunaj pravega časa starosti, ker je za zvestega imela njega, ki je bil obljubil.
12 Hivyo kutokana na huyu huyu ambaye alikuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
Zato jih je tudi od enega, in to umrlega, rodilo se kakor zvezd na nebu po številu, in kakor peska ob bregu morja bez števila.
13 Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
Poleg vere so umrli ti vsi, ko niso prejeli obljub; temuč videli so jih od daleč, in prepričani bili in pozdravili jih in spoznali, da so tujci in priseljenci na zemlji.
14 Watu wasemao mambo kama haya, wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
Kateri namreč tako govoré, naznanjajo, da iščejo domovine.
15 Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
In ko bi se bili spominjali one, iz katere so bili izšli, imeli bi bili čas obrniti se;
16 Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
Sedaj pa hrepené po boljši, to je, nebeški; zato se jih Bog ne sramuje imenovati se njih Boga; pripravil jim je namreč mesto.
17 Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaki kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu.
Po veri je daroval Abraham Izaka izkušan, in edinorojenca je daroval on, ki je bil prejel obljube, kateremu se je govorilo:
18 Ingawa Mungu alikuwa amemwambia Abrahamu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaki,”
"V Izaku se ti bode imenovalo seme;"
19 Abrahamu alihesabu kuwa Mungu angaliweza kumfufua Isaki kutoka kwa wafu. Na kwa kusema kwa mfano, alimpata tena Isaki kutoka kwa wafu.
Ker je pomislil, da more Bog tudi od mrtvih zbujati, od koder ga je tudi po priliki odnesel.
20 Kwa imani Isaki alimbariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
Po veri o prihodnjosti je Izak blagoslovil Jakoba in Ezava.
21 Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
Po veri je Jakob umirajoč blagoslovil slehernega izmed sinov Jožefovih in: "molil je na konci palice njegove."
22 Kwa imani, Yosefu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa wana wa Israeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
Po veri je Jožef umirajoč spominjal se izhoda sinov Izraelovih in naročal za kosti svoje.
23 Kwa imani, wazazi wa Mose walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
Po veri so Mojzesa rojenega roditelji skrivali tri mesece, ker so videli, da je dete zalo; in niso se bali ukaza kraljevega.
24 Kwa imani, Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
Po veri je Mojzes, ko je bil velik postal, branil se imenovan biti sin hčere Faraonove,
25 Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu.
Ker je raji hotel zlo trpeti z ljudstvom Božjim, nego imeti začasen užitek od greha;
26 Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Kristo ni utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
Ker je imel sramoto Kristusovo za večje bogastvo nad zaklade v Egiptu; kajti oziral se je v povračilo.
27 Kwa imani Mose aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
Po veri je zapustil Egipt, ne boječ se jeze kraljeve; stanoviten namreč je bil, kakor da bi videl nevidnega.
28 Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
Po veri je napravil pasho in polivanje s krvjo, da bi moritelj ne dotaknil se njih prvorojencev.
29 Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
Po veri so pregazili rudeče morje kakor po suhem; Egipčani pa poskusivši to bili so pogoltneni.
30 Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
Po veri je palo zidovje Jerihovo, okroženo sedem dnî.
31 Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
Po veri Rahab kurba ni poginila z nevernimi, sprejemši oglednike v miru.
32 Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii,
In kaj še govorim? Časa namreč mi bode primanjkovalo, ko bi pripovedoval o Gedeonu, Baraku in Samsonu in Jeftaji, Davidu in Samuelu in prerokih;
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
Kateri so po veri zmagovali kraljestva, delali pravico, dobivali obljube, levom žrela našili;
34 wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
Ognja moč gasili, meča osti ubežavali, od bolezni ozdravevali, junaki v vojski postajali, napade odbijali tujcev.
35 Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
Žene so dobivale po vstajenji mrtve svoje; drugi pa so bili mučeni, in niso sprejemali oproščenja, da zadobé boljše vstajenje;
36 Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
Drugi pa so poskusili zasramovanje in bičanje, in pa vezî in ječe;
37 Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
Bili so kamenjani, razrezani, izkušani, umrli so v smrti z mečem; hodili so v ovčjih, v kozjih kožah, v potrebi, v stiskah in težavah;
38 watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
(Njih ni bil vreden svet), po puščavah tavajoč in gorah in brlogih in podzemeljskih jamah.
39 Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
In vsi ti, pričanje prejemši po veri, niso dobili obljube,
40 Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.
Ker je bil Bog nekaj boljšega pred videl za nas, da bi se ne popolnili brez nas.

< Wahebrania 11 >