< Wahebrania 11 >

1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
Ora, a fé é o firme fundamento das coisas que se esperam, e a prova das coisas que se não vêem.
2 Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
Porque por ella os antigos alcançaram testemunho.
3 Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn g165)
Pela fé entendemos que os seculos pela palavra de Deus foram creados; de maneira que as coisas que se vêem não foram feitas das que se viam. (aiōn g165)
4 Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu bora zaidi kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
Pela fé Abel offereceu a Deus maior sacrificio do que Caim, pela qual alcançou testemunho de que era justo, porquanto Deus deu testemunho dos seus dons, e, depois de morto, ainda falla por ella.
5 Kwa imani Enoki alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
Pela fé Enoch foi trasladado para não ver a morte, e não foi achado, porquanto Deus o trasladara; porque antes da sua trasladação alcançou testemunho de que agradava a Deus.
6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.
Ora, sem fé é impossivel agradar a Deus: porque é necessario que aquelle que se approxima de Deus creia que elle existe, e que é galardoador dos que o buscam.
7 Kwa imani, Noa alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
Pela fé Noé, divinamente advertido das coisas que ainda se não viam, temeu, e, para salvação da sua familia, fabricou a arca, pela qual condemnou o mundo, e foi feito herdeiro da justiça que é segundo a fé.
8 Kwa imani Abrahamu, alipoitwa aende mahali ambapo Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakokwenda.
Pela fé Abrahão, sendo chamado, obedeceu, para sair ao logar que havia de receber por herança; e saiu, sem saber para onde ia
9 Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaki na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
Pela fé habitou na terra da promessa, como em terra alheia, morando em cabanas com Isaac e Jacob, herdeiros com elle da mesma promessa.
10 Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
Porque esperava a cidade que tem fundamentos, da qual o artifice e fabricador é Deus.
11 Kwa imani Abrahamu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
Pela fé tambem a mesma Sarah recebeu a virtude de conceber, e deu á luz já fóra da edade; porquanto teve por fiel aquelle que lh'o tinha promettido.
12 Hivyo kutokana na huyu huyu ambaye alikuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
Pelo que tambem de um, e esse já amortecido, nasceram em tão grande multidão como as estrellas do céu, e como a areia innumeravel que está na praia do mar.
13 Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
Todos estes morreram na fé, sem terem recebido as promessas; porém, vendo-as de longe, e crendo-as e abraçando-as, confessaram que eram estrangeiros e peregrinos na terra.
14 Watu wasemao mambo kama haya, wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
Porque os que isto dizem claramente mostram que buscam outra patria.
15 Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
E se, na verdade, se lembrassem d'aquella d'onde haviam saido, teriam tempo de tornar para ella.
16 Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
Mas agora desejam uma melhor, isto é, a celestial. Pelo que tambem Deus se não envergonha d'elles, de se chamar seu Deus, porque já lhes apparelhou uma cidade.
17 Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaki kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu.
Pela fé offereceu Abrahão a Isaac, quando foi provado; e aquelle que recebera as promessas offereceu o seu unigenito,
18 Ingawa Mungu alikuwa amemwambia Abrahamu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaki,”
Sendo-lhe dito: Em Isaac será chamada a tua descendencia; considerando que Deus era poderoso para até dos mortos o resuscitar.
19 Abrahamu alihesabu kuwa Mungu angaliweza kumfufua Isaki kutoka kwa wafu. Na kwa kusema kwa mfano, alimpata tena Isaki kutoka kwa wafu.
Por onde tambem em similhança o tornou a recobrar.
20 Kwa imani Isaki alimbariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
Pela fé Isaac abençoou Jacob e Esaú, no tocante ás coisas futuras.
21 Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
Pela fé Jacob, proximo da morte, abençoou cada um dos filhos de José, e adorou encostado á ponta do seu bordão.
22 Kwa imani, Yosefu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa wana wa Israeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
Pela fé José, proximo da morte, fez menção da saida dos filhos de Israel, e deu ordem ácerca de seus ossos.
23 Kwa imani, wazazi wa Mose walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
Pela fé Moysés, já nascido, foi escondido tres mezes por seus paes, porque viram que era um formoso menino; e não temeram o mandamento do rei
24 Kwa imani, Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
Pela fé Moysés, sendo já grande, recusou ser chamado filho da filha de Pharaó,
25 Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu.
Escolhendo antes ser maltratado com o povo de Deus de que por um pouco de tempo ter o gozo do peccado;
26 Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Kristo ni utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
Tendo por maiores riquezas o vituperio de Christo do que os thesouros do Egypto; porque tinha em vista a recompensa.
27 Kwa imani Mose aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
Pela fé deixou o Egypto, não temendo a ira do rei; porque esteve firme, como vendo o invisivel.
28 Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
Pela fé celebrou a paschoa e o derramamento de sangue, para que o destruidor dos primogenitos os não tocasse.
29 Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
Pela fé passaram o Mar Vermelho, como por terra secca; o que intentando os egypcios, se afogaram.
30 Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
Pela fé cairam os muros de Jericó, sendo sitiados durante sete dias.
31 Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
Pela fé Rahab, a meretriz, não pereceu com os incredulos, acolhendo em paz os espias.
32 Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii,
E que mais direi? Faltar-me-hia o tempo, contando de Gideon, e de Barac, e de Sansão, e de Jefthe, e de David, e de Samuel e dos prophetas:
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
Os quaes pela fé venceram reinos, exercitaram justiça, alcançaram promessas, fecharam as boccas dos leões,
34 wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
Apagaram a força do fogo, escaparam do fio da espada, da fraqueza tiraram forças, na batalha se esforçaram, pozeram em fugida os exercitos dos estranhos.
35 Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
As mulheres tornaram a receber pela resurreição os seus mortos, e outros foram estirados, não acceitando o seu livramento, para alcançarem uma melhor resurreição.
36 Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
E outros experimentaram escarneos e açoites, e até cadeias e prisões;
37 Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
Foram apedrejados, serrados, tentados, mortos ao fio da espada; andaram vestidos de pelles de ovelhas e de cabras, desamparados, afflictos e maltratados
38 watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
(Dos quaes o mundo não era digno), errantes pelos desertos, e montes, e covas e cavernas da terra.
39 Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
E todos estes, tendo testemunho pela fé, não alcançaram a promessa:
40 Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.
Provendo Deus alguma coisa melhor a nosso respeito, para que sem nós não fossem aperfeiçoados.

< Wahebrania 11 >