< Wahebrania 11 >
1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
Ent usk on kindel usaldus selle vastu, mida oodatakse, ja veendumus selles, mis pole veel nähtav.
2 Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
Selle usu kohta on meie esivanemad saanud hea tunnistuse.
3 Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn )
Usu kaudu me mõistame, et maailmad on valmistatud Jumala sõna läbi, nii et nähtamatust on sündinud nähtav. (aiōn )
4 Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu bora zaidi kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
Usus tõi Aabel Jumalale parema ohvri kui Kain. Selle tõttu tunnistas Jumal ta õigeks, kui Jumal kiitis heaks tema annid, ja usu kaudu kõneleb Aabel meile veel surnunagi.
5 Kwa imani Enoki alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
Usus võeti ära Eenok, nii et ta ei näinud surma: teda ei leitud enam, sest Jumal oli ta ära võtnud. Aga enne ülesvõtmist oli ta saanud tunnistuse, et ta oli Jumalale meelepärane.
6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.
Kuid ilma usuta on võimatu olla meelepärane. Sest igaüks, kes tuleb Jumala juurde, peab uskuma, et tema on olemas ja et ta annab palga neile, kes teda otsivad.
7 Kwa imani, Noa alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
Usu läbi sai Noa hoiatuse selle kohta, mida veel ei olnud näha, ja pühas kartuses ehitas ta laeva, millega pääses tema pere. Usu kaudu mõistis ta hukka maailma ja sai selle õiguse pärijaks, mis tuleb usust.
8 Kwa imani Abrahamu, alipoitwa aende mahali ambapo Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakokwenda.
Usus läks Aabraham kuulekalt teele, kui teda kutsuti paika, mille ta pidi saama pärandiks. Ta läks teele, teadmata, kuhu ta läheb.
9 Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaki na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
Usu läbi rajas ta oma kodu tõotatud maale otsekui sisserändaja võõrsile, elades telkides koos Iisaki ja Jaakobiga, kellele see tõotus samuti kuulus.
10 Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
Sest ta ootas kindlale vundamendile rajatud linna, mille kavandaja ja ehitaja on Jumal.
11 Kwa imani Abrahamu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
Ja usu läbi sai isegi viljatu Saara väe suguvõsa alustamiseks, kuigi oli sünnituseast juba ammu väljas, sest ta pidas tõotuse andjat ustavaks.
12 Hivyo kutokana na huyu huyu ambaye alikuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
Nii sündis ühest elujõu kaotanud mehest nõnda rohkesti järglasi, nagu on taevas tähti ja nagu merekaldal liiva, mida ei saa ära lugeda.
13 Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
Need kõik surid uskudes. Nad ei saanud kätte tõotusi, kuid nad nägid ja tervitasid neid eemalt. Ja nad tunnistasid, et nad on võõrad ja läbirändajad maa peal.
14 Watu wasemao mambo kama haya, wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
Sest kes nõnda räägivad, näitavad, et nad igatsevad kodumaad.
15 Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
Kui nad oleks meenutanud kodumaad, kust nad olid lahkunud, siis nad oleks saanud ju pöörduda tagasi.
16 Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
Aga nad igatsevad paremat, see tähendab taevast kodumaad. Seepärast Jumal ei häbene lasta end hüüda nende Jumalaks, kuna tema on valmistanud neile linna.
17 Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaki kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu.
Usu läbi Aabraham, kui Jumal ta proovile pani, loovutas ohvriks Iisaki; tema, kellele olid antud tõotused, tõi ohvrimäele oma ainsa poja,
18 Ingawa Mungu alikuwa amemwambia Abrahamu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaki,”
kuigi Jumal oli talle öelnud: „Sinu sugu loetakse Iisakist.“
19 Abrahamu alihesabu kuwa Mungu angaliweza kumfufua Isaki kutoka kwa wafu. Na kwa kusema kwa mfano, alimpata tena Isaki kutoka kwa wafu.
Aabraham leidis, et Jumal võib isegi surnuid üles äratada, ja selle võrdpildina sai ta Iisaki surmast tagasi.
20 Kwa imani Isaki alimbariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
Usus õnnistas ka Iisak Jaakobit ja Eesavit tulevaste asjade suhtes.
21 Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
Usus õnnistas surev Jaakob Joosepi mõlemat poega ja kummardas palves oma kepi najal.
22 Kwa imani, Yosefu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa wana wa Israeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
Usus meenutas Joosep oma elu lõpul Iisraeli laste lahkumist ja andis korralduse oma luude kohta.
23 Kwa imani, wazazi wa Mose walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
Usus varjasid Moosese vanemad pärast ta sündimist teda kolm kuud, sest nad nägid, et ta on ilus laps, ega kartnud teha kuninga käsu vastu.
24 Kwa imani, Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
Usus keeldus Mooses suureks saades laskmast end nimetada vaarao tütrepojaks,
25 Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu.
eelistades pigem taluda kurja kohtlemist koos Jumala rahvaga, kui nautida üürikest aega pattu.
26 Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Kristo ni utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
Ta pidas Egiptuse aardeist suuremaks rikkuseks teotust Kristuse pärast, sest ta kinnitas oma pilgu tulevasele tasule.
27 Kwa imani Mose aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
Usus lahkus ta Egiptusest, kartmata kuninga raevu, sest otsekui nähes teda, kes on nähtamatu, püsis ta kindlana.
28 Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
Usus korraldas ta paasapüha ja verega piserdamise uksepiitadele, et hävitusingel ei puutuks nende esmasündinuid.
29 Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
Usus läksid Iisraeli lapsed läbi Punase mere nagu kuiva maa, aga kui egiptlased üritasid sama, siis nad uppusid.
30 Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
Usus varisesid Jeeriko müürid, kui seitse päeva oli käidud nende ümber.
31 Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
Usus ei hukkunud hoor Raahab koos uskmatutega, sest ta oli rahuga vastu võtnud maakuulajad.
32 Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii,
Mida ma veel ütleksin? Mul puudub aeg hakata rääkima Gideonist, Baarakist, Simsonist, Jeftast, Taavetist, Saamuelist ja prohvetitest,
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
kes usu läbi vallutasid kuningriike, mõistsid kohut, said kätte tõotusi. Nad sulgesid lõvide lõuad,
34 wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
summutasid tule jõu, pääsesid mõõgatera eest, said nõtrusest tugevaks, osutusid vägevaks sõjas, lõid põgenema võõraste sõjahulgad.
35 Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
Naised said tagasi oma surnud ülestõusmise läbi. Teised lasksid end piinata surnuks, võtmata vastu pakutud vabadust ja eelistades paremat ülestõusmist.
36 Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
Teised said tunda jõhkrat pilkamist ja piitsahoope ning ahelaid vangikongis.
37 Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
Neid on visatud kividega surnuks, pooleks saetud, mõõgaga hukatud. Nad on käinud lamba- ja kitsenahas ja olnud puuduses, rõhutud, vaevatud –
38 watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
maailm ei olnud neid väärt. Nad ekslesid tühermaadel, mägedes, koobastes ja maalõhedes.
39 Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
Ja kuigi neid kõiki usu pärast kiideti, ei saanud nad kätte tõotust,
40 Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.
sest Jumal on midagi paremat kavandanud meie jaoks, et ainult koos meiega saaksid nad täiuslikuks.