< Wahebrania 10 >
1 Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
Car la Loi ayant l'ombre des biens à venir, et non la vive image des choses, ne peut jamais par les mêmes sacrifices que l'on offre continuellement chaque année, sanctifier ceux qui [s'y] attachent.
2 Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
Autrement n'eussent-ils pas cessé d'être offerts, puisque les sacrifiants étant une fois purifiés, ils n'eussent plus eu aucune conscience de péché?
3 Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
Or il y a dans ces [sacrifices] une commémoration des péchés réitérée d'année en année.
4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
Car il est impossible que le sang des taureaux et des boucs ôte les péchés.
5 Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
C'est pourquoi [Jésus-Christ] en entrant au monde a dit: tu n'as point voulu de sacrifice, ni d'offrande, mais tu m'as approprié un corps.
6 sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
Tu n'as point pris plaisir aux holocaustes, ni à l'oblation pour le péché.
7 Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
Alors j'ai dit: me voic, je viens, il est écrit de moi au commencement du Livre: que je fasse, ô Dieu ta volonté.
8 Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
Ayant dit auparavant: tu n'as point voulu de sacrifice, ni d'offrande, ni d'holocaustes, ni d'oblation pour le péché, et tu n'y as point pris plaisir, lesquelles choses sont [pourtant] offertes selon la Loi, alors il a dit: me voici, je viens afin de faire, ô Dieu! ta volonté!
9 Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
Il ôte [donc] le premier, afin d'établir le second.
10 Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
Or c'est par cette volonté que nous sommes sanctifiés, [savoir] par l'oblation qui a été faite une seule fois du corps de Jésus-Christ.
11 Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
Tout Sacrificateur donc assiste chaque jour, administrant, et offrant souvent les mêmes sacrifices, qui ne peuvent jamais ôter les péchés.
12 Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
Mais celui-ci ayant offert un seul sacrifice pour les péchés, s'est assis pour toujours à la droite de Dieu;
13 Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
Attendant ce qui reste, [savoir] que ses ennemis soient mis pour le marchepied de ses pieds.
14 kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
Car par une seule oblation, il a consacré pour toujours ceux qui sont sanctifiés.
15 Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
Et c'est aussi ce que le Saint-Esprit nous témoigne, car après avoir dit premièrement:
16 “Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
C'est ici l'alliance que je ferai avec eux après ces jours-là, dit le Seigneur, c'est que je mettrai mes Lois dans leurs cœurs, et je les écrirai dans leurs entendements;
17 Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
Et je ne me souviendrai plus de leurs péchés, ni de leurs iniquités.
18 Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
Or où les péchés sont pardonnés, il n'y a plus d'oblation pour le péché.
19 Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
Puis donc, mes frères, que nous avons la liberté d'entrer dans les lieux Saints par le sang de Jésus;
20 kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
[Qui est] le chemin nouveau et vivant qu'il nous a consacré; [que nous avons, dis-je, la liberté d'y entrer] par le voile, c'est-à-dire, par sa propre chair;
21 basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
Et [que nous avons] un grand Sacrificateur établi sur la maison de Dieu;
22 sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
Approchons-nous de lui avec un cœur sincère [et] une foi inébranlable, ayant les cœurs purifiés de mauvaise conscience, et le corps lavé d'eau nette;
23 Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
Retenons la profession de notre espérance sans varier, car celui qui [nous] a fait les promesses, est fidèle.
24 Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
Et prenons garde l'un à l'autre, afin de nous inciter à la charité et aux bonnes œuvres;
25 Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
Ne quittant point notre assemblée, comme quelques-uns ont accoutumé [de faire], mais nous exhortant [l'un l'autre; et] cela d'autant plus que vous voyez approcher le jour.
26 Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
Car si nous péchons volontairement après avoir reçu la connaissance de la vérité, il ne reste plus de sacrifice pour les péchés.
27 Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
Mais une attente terrible de jugement, et l'ardeur d'un feu qui doit dévorer les adversaires.
28 Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
Si quelqu'un avait méprisé la Loi de Moïse, il mourait sans miséricorde, sur la déposition de deux ou de trois témoins.
29 Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
De combien pires tourments pensez-vous [donc] que sera jugé digne celui qui aura foulé aux pieds le Fils de Dieu, et qui aura tenu pour une chose profane le sang de l'alliance, par lequel il avait été sanctifié, et qui aura outragé l'Esprit de grâce?
30 Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
Car nous connaissons celui qui a dit: c'est à moi que la vengeance appartient, et je [le] rendrai, dit le Seigneur. Et en-core: le Seigneur jugera son peuple.
31 Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
C'est une chose terrible que de tomber entre les mains du Dieu vivant.
32 Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
Or rappelez dans votre mémoire les jours précédents, durant lesquels après avoir été illuminés, vous avez soutenu un grand combat de souffrances;
33 Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
Ayant été d'une part exposés à la vue de tout le monde par des opprobres et des afflictions; et de l'autre, ayant participé [aux maux] de ceux qui ont souffert de semblables indignités.
34 Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
Car vous avez aussi été participants de l'affliction de mes liens, et vous avez reçu avec joie l'enlèvement de vos biens; sachant en vous-mêmes que vous avez dans les Cieux des biens meilleurs et permanents.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
Ne perdez point cette fermeté que vous avez fait paraître, et qui sera bien récompensée.
36 Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
Parce que vous avez besoin de patience, afin qu'après avoir fait la volonté de Dieu, vous receviez [l'effet de sa] promesse.
37 Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
Car encore un peu de temps, et celui qui doit venir, viendra, et il ne tardera point.
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
Or le juste vivra de la foi; mais si quelqu'un se retire, mon âme ne prend point de plaisir en lui.
39 Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.
Mais pour nous, nous n'avons garde de nous soustraire [à notre Maître]; ce serait notre perdition; mais nous persévérons dans la foi, pour le salut de l'âme.