< Wahebrania 10 >
1 Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
For the Torah, having a shadow of the good to come, not the very image of the things, can never with the same sacrifices year by year, which they offer continually, make perfect those who draw near.
2 Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
Or else wouldn’t they have ceased to be offered, because the worshippers, having been once cleansed, would have had no more consciousness of sins?
3 Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
But in those sacrifices there is a yearly reminder of sins.
4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
For it is impossible that the blood of bulls and goats should take away sins.
5 Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
Therefore when he comes into the world, he says, “You didn’t desire sacrifice and offering, but you prepared a body for me.
6 sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
You had no pleasure in whole burnt offerings and sacrifices for sin.
7 Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
Then I said, ‘Behold, I have come (in the scroll of the book it is written of me) to do your will, O God.’”
8 Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
Previously saying, “Sacrifices and offerings and whole burnt offerings and sacrifices for sin you didn’t desire, neither had pleasure in them” (those which are offered according to the Torah),
9 Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
then he has said, “Behold, I have come to do your will.” He takes away the first, that he may establish the second,
10 Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
by which will we have been sanctified through the offering of the body of Yeshua the Messiah once for all.
11 Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
Every priest indeed stands day by day serving and offering often the same sacrifices, which can never take away sins,
12 Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
but he, when he had offered one sacrifice for sins forever, sat down on the right hand of God,
13 Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
from that time waiting until his enemies are made the footstool of his feet.
14 kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
For by one offering he has perfected forever those who are being sanctified.
15 Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
The Holy Spirit also testifies to us, for after saying,
16 “Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
“This is the covenant that I will make with them after those days,” says the Lord, “I will put my laws on their heart, I will also write them on their mind;” then he says,
17 Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
“I will remember their sins and their iniquities no more.”
18 Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
Now where remission of these is, there is no more offering for sin.
19 Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
Having therefore, brothers, boldness to enter into the holy place by the blood of Yeshua,
20 kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
by the way which he dedicated for us, a new and living way, through the veil, that is to say, his flesh,
21 basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
and having a great priest over God’s house,
22 sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
let’s draw near with a true heart in fullness of faith, having our hearts sprinkled from an evil conscience and having our body washed with pure water,
23 Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
let’s hold fast the confession of our hope without wavering; for he who promised is faithful.
24 Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
Let’s consider how to provoke one another to love and good works,
25 Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
not forsaking our own assembling together, as the custom of some is, but exhorting one another, and so much the more as you see the Day approaching.
26 Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For if we sin wilfully after we have received the knowledge of the truth, there remains no more a sacrifice for sins,
27 Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
but a certain fearful expectation of judgement, and a fierceness of fire which will devour the adversaries.
28 Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
A man who disregards the Torah of Moses dies without compassion on the word of two or three witnesses.
29 Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
How much worse punishment do you think he will be judged worthy of who has trodden under foot the Son of God, and has counted the blood of the covenant with which he was sanctified an unholy thing, and has insulted the Spirit of grace?
30 Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
For we know him who said, “Vengeance belongs to me. I will repay,” says the Lord. Again, “The Lord will judge his people.”
31 Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
It is a fearful thing to fall into the hands of the living God.
32 Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
But remember the former days, in which, after you were enlightened, you endured a great struggle with sufferings:
33 Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
partly, being exposed to both reproaches and oppressions, and partly, becoming partakers with those who were treated so.
34 Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
For you both had compassion on me in my chains and joyfully accepted the plundering of your possessions, knowing that you have for yourselves a better possession and an enduring one in the heavens.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
Therefore don’t throw away your boldness, which has a great reward.
36 Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
For you need endurance so that, having done the will of God, you may receive the promise.
37 Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
“In a very little while, he who comes will come and will not wait.
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
But the righteous one will live by faith. If he shrinks back, my soul has no pleasure in him.”
39 Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.
But we are not of those who shrink back to destruction, but of those who have faith to the saving of the soul.