< Wahebrania 10 >

1 Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
For the lawe which hath but the shadowe of good thynges to come and not the thynges in their awne fassion can never with ye sacryfises which they offer yere by yere continually make the comers thervnto parfayte.
2 Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
For wolde not then those sacrifises have ceased to have bene offered because that the offerers once pourged shuld have had no moare conscieces of sinnes.
3 Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
Neverthelesse in those sacrifises is ther mencion made of synnes every yeare.
4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
For it is vnpossible that the bloud of oxen and of gotes shuld take awaye synnes.
5 Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
Wherfore when he commeth into the worlde he sayth: Sacrifice and offeringe thou woldest not have: but a bodie hast thou ordeyned me.
6 sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
In sacrifices and synne offerynges thou hast no lust.
7 Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
Then I sayde: Lo I come in the chefest of the boke it is written of me that I shuld doo thy will o god.
8 Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
Above when he had sayed sacrifice and offerynge and burnt sacrifices and synne offerynges thou woldest not have nether hast alowed (which yet are offered by the lawe)
9 Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
and then sayde: Lo I come to do thy will o god: he taketh awaye the fyrst to stablisshe the latter.
10 Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
By the which will we are sanctified by the offeringe of the body of Iesu Christe once for all.
11 Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
And every prest is redy dayly ministrynge and ofte tymes offereth one maner of offerynge which can never take awaye synnes.
12 Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
But this man after he had offered one sacrifyce for synnes sat him doune for ever on the right honde of god
13 Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
and from hence forth tarieth till his foes be made his fotestole.
14 kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
For with one offerynge hath he made parfecte for ever them yt are sanctified.
15 Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
And ye holy goost also beareth vs recorde of this even when he tolde before:
16 “Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
This is the testament that I will make vnto them after those dayes sayth the lorde. I will put my lawes in their hertes and in their mynde I will write them
17 Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
and their synnes and iniquyties will I remember no moare.
18 Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
And where remission of these thinges is there is no moare offerynge for synne.
19 Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
Seynge brethren that by the meanes of the bloud of Iesu we maye be bolde to enter into that holy place
20 kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
by the newe and livynge waye which he hath prepared for vs through the vayle that is to saye by his flesshe.
21 basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
And seynge also that we have an hye prest which is ruler over ye housse of god
22 sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
let vs drawe nye with a true herte in a full fayth sprynckeled in oure hertes from an evyll conscience and wesshed in oure bodies with pure water
23 Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
and let vs kepe the profession of oure hope with oute waveringe (for he is faythfull that promysed)
24 Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
and let vs consyder one another to provoke vnto love and to good workes:
25 Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
and let vs not forsake the felishippe that we have amoge oure selves as the maner of some is: but let vs exhorte one another and that so moche the more because ye se that the daye draweth nye.
26 Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For yf we synne willyngly after that we have receaved the knowledge of the trueth there remayneth no more sacrifice for synnes
27 Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
but a fearfull lokynge for iudgement and violent fyre which shall devoure the adversaries
28 Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
He that despiseth Moses lawe dyeth with out mercy vnder two or thre witnesses.
29 Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
Of how moche sorer punyshment suppose ye shall he be counted worthy which treadeth vnderfote the sonne of god: and counteth the bloude of the testament as an vnholy thynge wherwith he was sanctified and doth dishonoure to the sprete of grace.
30 Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
For we knowe him that hath sayde vengeaunce belongeth vnto me I will recompence sayth the lorde. And agayne: the lorde shall iudge his people.
31 Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
It is a fearfull thynge to faule into the hondes of the livynge God.
32 Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
Call to remebraunce the dayes that are passed in the which after ye had receaved light ye endured a greate fyght in adversities
33 Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
partly whill all men wondred and gased at you for the shame and trioulacion that was done vnto you and partly whill ye became companyons of the which so passed their tyme.
34 Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
For ye suffered also with my bondes and toke a worth the spoylynge of youre goodes and that with gladnes knowynge in youre selves how that ye had in heven a better and an endurynge substaunce
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
Cast not awaye therfore youre confidence which hath great rewarde to recopence.
36 Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
For ye have nede of paciece that after ye have done ye will of god ye myght receave the promes.
37 Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
For yet a very lytell whyle and he that shall come will come and will not tary.
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
But the iust shall live by faith. And yf he withdrawe him silfe my soule shall have no pleasure in him.
39 Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.
We are not whiche withdrawe oure selves vnto dampnacio but partayne to fayth to the wynnynge of the soule.

< Wahebrania 10 >