< Wahebrania 10 >
1 Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
For the Law but shadowing forth the good things to come, and not having the very image of the things, can never with the same sacrifices which they offer year by year continually make those who come with them perfect.
2 Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
For in that case would they not have ceased to be offered, because the worshippers, having been once purified, would have had no more consciousness of sins?
3 Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
But in these sacrifices there is a remembrance of sins every year.
4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
For it is impossible that the blood of bulls and goats should take away sins.
5 Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
Wherefore, when he cometh into the world, he saith: “Sacrifice and offering thou wouldest not, but a body didst thou prepare for me;
6 sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
in whole burnt-offerings and sacrifices for sin thou hadst no pleasure.
7 Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
Then said I, Lo, I have come—in the volume of the book it is written of me—to do thy will, O God.”
8 Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
Saying above, “Sacrifices and offerings, and whole burnt-offerings and sacrifices for sin thou wouldest not, and hadst no pleasure in them,”—such as are offered in conformity to the Law, —
9 Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
then hath he said, “Lo, I have come to do thy will.” He setteth aside the first, that he may establish the second.
10 Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
And in this will we have been sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once for all.
11 Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
And every priest indeed standeth performing daily service, and offering again and again the same sacrifices, which can never take away sins;
12 Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
but he, after he had offered one sacrifice for sins, sat down for ever on the right hand of God,
13 Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
thenceforth waiting until his enemies be made his footstool.
14 kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
For by one offering he hath perfected for ever those who are sanctified.
15 Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
Moreover the Holy Spirit also is a witness to us of this. For after he had said,
16 “Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
“This is the covenant that I will make with them after those days,” the Lord saith, “I will put my laws into their hearts, and in their minds will I write them,
17 Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
and their sins and iniquities will I remember no more.”
18 Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
But where there is remission of these, there is no longer offering for sin.
19 Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
Having therefore, brethren, boldness for entrance into the sanctuary by the blood of Jesus,
20 kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
a new and living way, which he consecrated for us, through the veil, that is, his flesh,
21 basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
and having a great priest over the house of God,
22 sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
let us draw near with a true heart in full assurance of faith, having had our hearts sprinkled from an evil conscience; and having had our bodies washed with pure water,
23 Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
let us hold fast the profession of our hope without wavering, for he is faithful who promised;
24 Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
and let us consider one another, to excite to love and to good works,
25 Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
not forsaking the assembling of ourselves together, as the custom of some is, but exhorting one another; and so much the more, as ye see the day approaching.
26 Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For if we sin willingly after we have received the knowledge of the truth, there no longer remaineth a sacrifice for sins;
27 Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
but a certain fearful looking for judgment, and an indignation by fire, which will devour the adversaries.
28 Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
He that hath set at nought the law of Moses dieth without mercy under two or three witnesses;
29 Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
of how much heavier punishment, think ye, will he be thought worthy, who hath trodden under foot the Son of God, and hath counted the blood of the covenant, wherewith he was sanctified, an unholy thing, and hath done despite to the Spirit of grace?
30 Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
For we know him who said, “Vengeance belongeth to me, I will recompense, saith the Lord;” and again, “The Lord will judge his people.”
31 Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
It is a fearful thing to fall into the hands of the living God.
32 Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
But call to remembrance the former days, in which, after ye were enlightened, ye endured a great struggle with sufferings;
33 Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
partly, while ye were made a gazing-stock both by reproaches and afflictions; and partly, while ye became partakers with those that were so used.
34 Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
For ye sympathized with those in bonds, and ye took joyfully the plundering of your goods, knowing that ye have for yourselves a better and an enduring substance.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
Cast not away therefore your confidence, which hath great recompense of reward.
36 Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
For ye have need of endurance; that, after ye have done the will of God, ye may receive what is promised.
37 Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
For yet a very little while, and “he that is to come will come, and will not tarry.
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
Now my righteous man shall live by faith; but if he draw back, my soul hath no pleasure in him.”
39 Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.
But we are not of those who draw back, unto perdition; but of those who believe, to the saving of the soul.