< Wahebrania 1 >
1 Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
Kui Jumal muiste rääkis esivanematele mitmel korral ja mitmel viisil prohvetite kaudu,
2 lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn )
siis on Jumal viimseil päevil meile rääkinud Poja kaudu, kelle ta on seadnud kõigi asjade pärijaks ja kelle läbi ta on ka maailmad loonud. (aiōn )
3 Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
Poeg on Jumala kirkuse kiirgus ja tema olemuse täpne peegeldus ning ta hoiab ülal kõiksust oma võimsa sõnaga. Kes on pärast seda, kui ta oli puhastanud meid pattudest, istunud Ausuuruse paremale käele kõrgustes
4 Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
ning saanud ülemaks inglitest, kuivõrd ta on pärinud neist ülevama nime.
5 Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
Millisele inglile on Jumal iganes öelnud „Sina oled minu Poeg, täna ma sünnitasin sinu“? Ja veel: „Mina olen tema Isa ja tema on minu Poeg.“
6 Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
Ning kui ta toob oma esmasündinu maailma, ütleb ta: „Teda kummardagu kõik Jumala inglid.“
7 Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
Inglite kohta ta ütleb: „Ta teeb oma inglid vaimudeks, ja oma teenijad tuleleegiks.“
8 Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn )
Aga Poja kohta ta ütleb: „Sinu troon, Jumal, püsib ikka ja igavesti, ja õiglus on su Kuningriigi valitsuskepp. (aiōn )
9 Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
Sa armastad õigust ja vihkad ülekohut, seepärast on su Jumal võidnud sind rõõmuõliga rohkem kui su kaaslasi.“
10 Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
Ja veel: „Sina, Issand, panid alguses maale aluse ja taevad on su kätetöö.
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
Need hävivad, aga sina jääd; nad kõik kuluvad nagu riie.
12 Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
Sa keerad nad kokku otsekui kuue – nad vahetatakse välja nagu rõivad. Ent sina oled ikka seesama ja sinu aastad ei lõpe.“
13 Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
Või millisele inglile on Jumal iganes öelnud: „Istu mu paremale käele, kuni ma panen sinu vaenlased su jalajäriks“?
14 Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?
Eks kõik inglid ole teenijad vaimud, saadetud teenima neid, kes pärivad pääste?