< Wahebrania 1 >

1 Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
On many occasions and in many ways in the olden time, God having spoken to the fathers through the prophets, at the last of these days has spoken to us through his Son,
2 lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn g165)
whom he put forth the heir of all things, and through whom he created the ages; (aiōn g165)
3 Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
who being the brightness of his glory, and the character of his person, and holding up all things by the word of his power, having made purgation of the sins, sat down on the right hand of the Majesty on high;
4 Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
being so much greater than the angels, that he has inherited a name so much more excellent than they.
5 Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
For to which one of the angels at any time did he say, Thou art my Son, this day have I begotten thee? and again, I will be unto him a Father, and he shall be unto me a Son?
6 Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
And again when he may lead in the first begotten into the world, he says, Indeed let all the angels of God worship him.
7 Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
And to the angels he says, he maketh his angels spirits, and his ministers a flame of fire: but to the Son he says,
8 Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn g165)
Thy throne, O God, is unto the age of the age; and the scepter of righteousness is the scepter of thy kingdom. (aiōn g165)
9 Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
Thou hast loved righteousness, and hated iniquity; therefore God, thy God, has anointed thee with the oil of gladness above thy comrades.
10 Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
And thou, at the beginning, O Lord, didst lay the foundations of the earth, and the heavens are the works of thy hands.
11 Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
These shall perish; but thou dost remain: truly all these shall wax old like a garment;
12 Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
and thou shalt roll them up like a mantle, and they shall be changed: but thou art the same, and thy years shall not fail thee.
13 Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
And to which one of the angels has he at any time said, Sit thou on my right hand, until I may make thine enemies the footstool of thy feet?
14 Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?
Are not all these ministering spirits, having been sent forth unto ministration for the sake of those who are about to inherit salvation?

< Wahebrania 1 >