< Hagai 1 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
در سال دوم سلطنت داریوش، در روز اول ماه ششم، خداوند پیامی توسط حَجَّی نبی برای زروبابِل (پسر شئلتیئیل) حاکم یهودا، و برای یهوشع (پسر یهوصادق) کاهن اعظم، فرستاد.
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
خداوند لشکرهای آسمان به حَجَّی نبی فرمود: «این قوم می‌گویند که اکنون وقت بازسازی خانهٔ خدا نیست.»
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
سپس، خداوند این پیام را توسط حَجَّی نبی برای قوم فرستاد:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
«آیا این درست است که شما در خانه‌های نوساخته زندگی کنید ولی خانهٔ من خراب بماند؟
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
پس حال خداوند لشکرهای آسمان چنین می‌گوید: به نتیجهٔ کارهایتان نگاه کنید:
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
بذر زیاد می‌کارید، ولی محصول کم برداشت می‌کنید؛ می‌خورید ولی سیر نمی‌شوید؛ می‌نوشید ولی تشنگی‌تان رفع نمی‌گردد؛ لباس می‌پوشید اما گرم نمی‌شوید؛ مزد می‌گیرید ولی گویی آن را در کیسه‌های سوراخ می‌گذارید.
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
«خداوند لشکرهای آسمان چنین می‌گوید: خوب فکر کنید و ببینید چه کرده‌اید و نتیجه‌اش چه بوده است!
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
حال به کوه رفته، چوب بیاورید و خانهٔ مرا دوباره بسازید تا من از آن راضی شوم و در آنجا مردم احترام مرا بجا آورند.
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
«انتظار محصول فراوانی داشتید، اما خیلی کم به دست آوردید؛ و وقتی همان مقدار کم را هم به منزل آوردید، آن را از بین بردم. می‌دانید چرا؟ خداوند لشکرهای آسمان می‌فرماید: چون خانهٔ من خراب مانده و شما فقط به فکر خانه‌های خود هستید.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
به همین علّت است که آسمان نمی‌بارد و زمین محصول خود را نمی‌دهد.
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
من در سرزمین شما خشکسالی پدید آورده‌ام و این خشکسالی تمام کوهها، مزرعه‌ها، تاکستانها، باغهای زیتون و سایر محصولات و حتی انسان و حیوان و تمام حاصل دسترنج شما را فرا خواهد گرفت.»
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
آنگاه زروبابِل و یهوشع و تمام کسانی که از اسارت برگشته بودند از خداوند ترسیدند و پیام حَجَّی نبی را که خداوند، خدایشان به او داده بود اطاعت کردند.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
سپس خداوند بار دیگر توسط نبی خود حَجَّی به قوم فرمود: «من با شما هستم.»
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
خداوند روحِ زَروبابِل فرزند شِئَلتیئیل فرماندار یهودا، و روحِ یِهوشَع فرزند یِهوصاداق کاهن اعظم، و روح تمامی باقیماندگان قوم را برانگیخت تا خانهٔ یهوه خدای خود، خدای لشکرهای آسمان، را بسازند.
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
پس، در سال دوم سلطنت داریوش در روز بیست و چهارم ماه ششم خانۀ خداوند ساخته شد.

< Hagai 1 >