< Hagai 1 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
La seconde année du roi Darius, le premier jour du sixième mois, la parole de l'Éternel fut adressée, par Aggée, le prophète, à Zorobabel, fils de Salathiel, gouverneur de Juda, et à Joshua, fils de Jotsadak, grand sacrificateur, en ces termes:
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
Ainsi a parlé l'Éternel des armées, en disant: Ce peuple dit: Le temps n'est pas venu, le temps de rebâtir la maison de l'Éternel.
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
Et la parole de l'Éternel fut adressée, par Aggée, le prophète, en ces mots:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
Est-il temps pour vous d'habiter dans des maisons lambrissées, pendant que cette maison-là est en ruine?
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Maintenant donc, ainsi a dit l'Éternel des armées: Considérez attentivement vos voies.
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
Vous avez semé beaucoup, mais peu recueilli; vous mangez, mais vous n'êtes pas rassasiés; vous buvez, mais vous n'êtes pas désaltérés; vous êtes vêtus, mais vous n'êtes pas réchauffés; et celui qui gagne met son salaire dans un sac percé.
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Ainsi a dit l'Éternel des armées: Considérez attentivement vos voies.
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
Montez à la montagne, apportez du bois, et bâtissez la maison: j'y prendrai plaisir, et je serai glorifié, dit l'Éternel.
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
Vous comptiez sur beaucoup, et voici, il y a eu peu; vous l'avez porté chez vous, mais j'ai soufflé dessus. Pourquoi? dit l'Éternel des armées. A cause de ma maison, parce qu'elle reste en ruine, pendant que vous vous empressez chacun pour sa maison.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
C'est pourquoi les cieux au-dessus de vous retiennent la rosée, et la terre retient son produit.
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
Et j'ai appelé la sécheresse sur la terre, et sur les montagnes, et sur le blé, sur le moût et sur l'huile, et sur tout ce que le sol produit, et sur les hommes et sur les bêtes, et sur tout le travail des mains.
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
Zorobabel, fils de Salathiel, Joshua, fils de Jotsadak, grand sacrificateur, et tout le reste du peuple entendirent la voix de l'Éternel, leur Dieu, et les paroles d'Aggée, le prophète, selon la mission que lui avait donnée l'Éternel leur Dieu; et le peuple eut de la crainte devant l'Éternel.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
Et Aggée, envoyé de l'Éternel, parla au peuple selon le message de l'Éternel, disant: Je suis avec vous, dit l'Éternel.
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
Et l'Éternel excita l'esprit de Zorobabel, fils de Salathiel, gouverneur de Juda, et l'esprit de Joshua, fils de Jotsadak, grand sacrificateur, et l'esprit de tout le reste du peuple; et ils vinrent, et se mirent à travailler à la maison de l'Éternel des armées, leur Dieu,
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
Le vingt-quatrième jour du sixième mois, la seconde année du roi Darius.

< Hagai 1 >