< Hagai 1 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
La deuxième année du roi Darius, le sixième mois, le premier jour du mois, la parole de Yahvé fut adressée par Aggée, le prophète, à Zorobabel, fils de Shealtiel, gouverneur de Juda, et à Josué, fils de Jotsadak, le grand prêtre, en ces termes:
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
« Voici ce que dit Yahvé des armées: Ce peuple dit: 'Le temps n'est pas encore venu, le temps de construire la maison de Yahvé'. »
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
Et la parole de Yahvé vint par Aggée, le prophète, en ces termes:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
Est-ce le moment pour vous d'habiter dans vos maisons à pan coupé, tandis que cette maison est détruite?
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Voici donc ce que dit l'Éternel des armées: « Considérez vos voies.
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
Vous avez beaucoup semé, et vous rapportez peu. Vous mangez, mais vous n'avez pas assez. Vous buvez, mais vous n'êtes pas rassasiés. Vous vous habillez, mais personne n'a chaud; et celui qui gagne un salaire le gagne pour le mettre dans un sac troué.''
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Voici ce que dit l'Éternel des armées: « Considère tes voies.
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
Monte sur la montagne, apporte du bois, et construis la maison. J'y prendrai plaisir, et je serai glorifié, dit l'Éternel.
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
Tu as cherché beaucoup, et voici qu'il n'y a eu que peu de choses; et quand tu l'as rapportée à la maison, je l'ai soufflée. Pourquoi? dit l'Éternel des armées, à cause de ma maison qui gît, tandis que chacun de vous est occupé de sa propre maison.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
C'est pourquoi, à cause de vous, les cieux retiennent la rosée, et la terre retient ses fruits.
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
J'ai appelé la sécheresse sur la terre, sur les montagnes, sur le blé, sur le vin nouveau, sur l'huile, sur ce que produit le sol, sur les hommes, sur le bétail, et sur tout le travail des mains. »
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
Et Zorobabel, fils de Shealtiel, et Josué, fils de Jehozadak, le grand prêtre, et tout le reste du peuple, obéirent à la voix de Yahvé, leur Dieu, et aux paroles du prophète Aggée, comme Yahvé, leur Dieu, l'avait envoyé; et le peuple craignit Yahvé.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
Alors Aggée, le messager de Yahvé, transmit au peuple le message de Yahvé, en disant: « Je suis avec vous, dit Yahvé.
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
L'Éternel réveilla l'esprit de Zorobabel, fils de Schealthiel, gouverneur de Juda, l'esprit de Josué, fils de Jotsadak, le souverain sacrificateur, et l'esprit de tout le reste du peuple; et ils vinrent travailler à la maison de l'Éternel des armées, leur Dieu,
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
le vingt-quatrième jour du mois, le sixième mois, la seconde année du roi Darius.

< Hagai 1 >