< Hagai 1 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
In the second year of Darius the king, on the first day of the sixth month, this message from the Lord came through Haggai the prophet to Zerubbabel the son of Shealtiel, governor of Judah, and to Joshua the son of Jehozadak, the high priest:
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
The Lord of hosts says: The people say that the time has not yet come to rebuild the temple of the Lord.
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
Then this message from the Lord came to Haggai the prophet:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
Is it a time for you yourselves to live in your own well-roofed houses, while this temple lies in ruins?
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
The Lord of hosts says: Consider your past experiences.
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
You sow much, but bring in little; you eat, but you do not have enough; you drink, but are not filled; you clothe yourselves, but not enough to be warm; and those who earn wages, put those wages in a bag with holes.
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
The Lord of hosts says: Consider your experiences.
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
Go up to the mountains, and bring wood and rebuild the temple; then I will be pleased with it, and I will reveal my glory. The Lord says:
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
You looked for much, and it came to little; and when you brought the harvest home, I blew it away. Why? The Lord of hosts says: Because my temple lies in ruins, while you shelter in your own houses.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
The heavens withhold the dew, and the earth withholds its fruit,
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
and I have called forth a drought upon the land and upon the mountains, and upon the grain and the new wine and the oil and upon that which the ground brings forth, and upon people and animals, and upon all the labor of your hands.
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
Then Zerubbabel the son of Shealtiel and Joshua the son of Jehozadak the high priest, with all the rest of the people, obeyed the command of the Lord their God and the words of Haggai the prophet, as the Lord their God had sent him to them. They showed proper respect for the Lord.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
Haggai, the prophet of the Lord, as the Lord commanded him, told the people: “The Lord says: I am with you.”
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
And the Lord stirred up the spirit of Zerubbabel the son of Shealtiel, governor of Judah, and the spirit of Joshua the son of Jehozadak the high priest, and the spirit of all the rest of the people, so that they came and worked on the temple of the Lord of hosts, their God,
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
in the twenty-fourth day of the sixth month. In the second year of Darius the king,