< Hagai 2 >

1 Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
No sétimo mês, no vigésimo primeiro dia do mês, a palavra de Javé veio pelo profeta Ageu, dizendo:
2 “Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
“Fale agora com Zerubabel, filho de Shealtiel, governador de Judá, e com Josué, filho de Jehozadak, o sumo sacerdote, e com o resto do povo, dizendo:
3 ‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
'Quem ficou entre vós que viu esta casa em sua antiga glória? Como vocês a vêem agora? Não está em seus olhos como nada?
4 Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Ainda agora seja forte, Zerubbabel', diz Yahweh. Seja forte, Josué, filho de Jehozadak, o sumo sacerdote”. Sejam fortes, todos vocês da terra', diz Javé, 'e trabalhem, pois estou com vocês', diz Javé dos Exércitos.
5 ‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
Esta é a palavra que eu fiz convênio com vocês quando saíram do Egito, e meu Espírito viveu entre vocês. 'Não tenha medo'.
6 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
Pois isto é o que diz Javé dos Exércitos: 'Ainda uma vez mais, é um pouco de tempo, e sacudirei os céus, a terra, o mar e a terra seca;
7 Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
e sacudirei todas as nações'. O tesouro de todas as nações virá, e eu encherei esta casa de glória, diz Yahweh dos Exércitos.
8 ‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
A prata é minha, e o ouro é meu', diz Javé dos Exércitos.
9 ‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
'A última glória desta casa será maior do que a primeira', diz Javé dos Exércitos; 'e neste lugar darei a paz', diz Javé dos Exércitos”.
10 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
No vigésimo quarto dia do nono mês, no segundo ano de Dario, a palavra de Javé veio do profeta Ageu, dizendo:
11 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
“diz Javé dos Exércitos: Pergunta agora aos sacerdotes a respeito da lei, dizendo:
12 Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
'Se alguém carrega carne santa na prega de sua roupa, e com sua prega toca o pão, o guisado, o vinho, o óleo, ou qualquer comida, ela se tornará santa...'”. Os padres responderam: “Não”.
13 Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
Então Haggai disse: “Se alguém que está impuro por causa de um cadáver tocar em algum destes, será que está impuro? Os padres responderam: “Será impuro”.
14 Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
Então Haggai respondeu: “'Assim é este povo, e assim é esta nação diante de mim', diz Yahweh; 'e assim é todo trabalho de suas mãos. O que eles oferecem ali é impuro”.
15 “‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
Agora, por favor, considere a partir deste dia e para trás, antes que uma pedra fosse colocada sobre uma pedra no templo de Yahweh.
16 Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
Durante todo esse tempo, quando se chegava a um monte de vinte medidas, havia apenas dez. Quando se chegava a uma cuba de vinho para tirar cinqüenta, eram apenas vinte.
17 Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
Eu o golpeei com ferrugem, mofo e granizo em todo o trabalho de suas mãos; no entanto, você não se voltou para mim”, diz Yahweh.
18 ‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
'Considere, por favor, a partir deste dia e para trás, a partir do vigésimo quarto dia do nono mês, desde o dia em que a fundação do templo de Yahweh foi lançada, considere-o.
19 Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
A semente já se encontra no celeiro? Sim, a videira, a figueira, a romãzeira e a oliveira ainda não produziram. A partir de hoje, eu os abençoarei”.
20 Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
A palavra de Javé veio pela segunda vez ao Ageu no vigésimo quarto dia do mês, dizendo:
21 “Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
“Fale com Zerubbabel, governador de Judá, dizendo: 'Eu sacudirei os céus e a terra'.
22 Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
I derrubará o trono dos reinos”. Destruirei a força dos reinos das nações”. Derrubarei as carruagens e os que nelas cavalgam”. Os cavalos e seus cavaleiros descerão, todos pela espada de seu irmão.
23 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
Naquele dia, diz Javé dos Exércitos, eu te levarei, Zerubbabel meu servo, o filho de Shealtiel', diz Javé, 'e te farei como um anel de sinete, pois eu te escolhi', diz Javé dos Exércitos”.

< Hagai 2 >