< Hagai 2 >
1 Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
Et le vingt-unième jour du septième mois, le Seigneur confia Sa parole aux mains d'Aggée, le prophète, disant:
2 “Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
Parle à Zorobabel, fils de Salathiel, de la tribu de Juda, et à Jésus, fils de Josédec, le grand prêtre, et à tout le reste du peuple, disant:
3 ‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
Qui de vous a vu ce temple en sa première gloire? Et comment le voyez-vous aujourd'hui? N'est-il pas devant vous comme n'étant point?
4 Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Et maintenant arme-toi de force, Zorobabel, fils de Salathiel, de la tribu de Juda; arme-toi de force, Jésus, fils de Josédec, le grand-prêtre; arme-toi de force, peuple de la terre, dit le Seigneur, et travaille; car Je suis avec vous, dit le Seigneur tout-puissant.
5 ‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
Et Mon Esprit est debout au milieu de vous; ayez confiance;
6 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
Car voici ce que dit le Seigneur tout-puissant: Encore une fois, J'ébranlerai le ciel et la terre, la mer et le désert;
7 Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
et J'ébranlerai toutes les nations; et celles des nations que J'aurai élevées viendront; et je remplirai de gloire le temple, dit le Seigneur tout- puissant.
8 ‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
À Moi est l'or, à Moi l'argent, dit le Seigneur tout-puissant.
9 ‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
La gloire de ce temple sera grande; mais celle de la fin surpassera celle du commencement, dit le Seigneur Dieu tout-puissant; et à cette terre Je donnerai la paix, dit le Seigneur Dieu tout-puissant, et je donnerai la paix en ce lieu à tous ceux qui travaillent à réédifier le temple.
10 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
Le vingt-troisième jour du neuvième mois de la seconde année du règne de Darius, la parole du Seigneur vint à Aggée, le prophète, disant:
11 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
Voici ce que dit le Seigneur, Maître de toutes choses: Consulte les prêtres sur la loi; dis-leur:
12 Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
Si un homme prend dans le coin de son manteau de la chair consacrée, et si le coin de son manteau touche du pain ou de la viande cuite, du vin ou de l'huile, ou tout autre aliment, cet aliment sera-t-il sanctifié? Et les prêtres répondirent et dirent: Non.
13 Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
Et Aggée dit: Si un homme souillé et non purifié en son âme touche l'une de ces choses, sera-t-elle souillée? Et les prêtres répondirent et dirent: Elle sera souillée.
14 Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
Et Aggée reprit, et dit: Tel est ce peuple; telle est cette nation devant Moi, dit le Seigneur; telles sont toutes les œuvres de leurs mains; tel est celui qui approchera de ce lieu souillé à cause des présents qu'il a reçus le matin; et ils souffriront à l'aspect de leurs travaux; et ils ont haï celui qui les a réprimandés devant les portes de la ville.
15 “‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
Et maintenant, en vos cœurs, remontez dans le passé à partir de ce jour, avant qu'on eût posé pierre sur pierre dans le temple du Seigneur; ce qui vous arrivait
16 Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
lorsque vous jetiez dans le coffre à orge vingt mesures de grain, et qu'elles se réduisaient à dix; lorsque vous alliez à la cuve, sous le pressoir, pour y puiser vingt-cinq mesures, et qu'il n'y en avait plus que vingt.
17 Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
Je vous ai frappés par la stérilité; J'ai frappé les œuvres de vos mains par les ravages du vent et par la grêle; et vous ne vous êtes point convertis à Moi, dit le Seigneur.
18 ‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
Pensez donc en vos cœurs, à partir de ce jour et au delà, à partir du vingt-troisième jour du neuvième mois, et du jour où le temple du Seigneur a été fondé; considérez en vos cœurs
19 Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
si l'on voit pareille chose dans les granges; vigne, figuier, grenadier ou olivier, rien n'a encore porté des fruits; mais à partir de ce jour Je vous bénirai.
20 Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
Et la parole du Seigneur vint une seconde fois à Aggée, le prophète, le vingt-quatrième jour du moi, disant:
21 “Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
Parle à Zorobabel, fils de Salathiel, de la tribu de Juda; dis-lui J'ébranlerai le ciel et la terre, la mer et le désert,
22 Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
et Je renverserai le trône des rois, et Je détruirai la puissance des rois des nations, et je ferai tomber leurs chars et leurs écuyers; et les chevaux et leurs cavaliers seront abattus; et le frère frappera du glaive son frère.
23 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
Or, en ce jour-là, dit le Seigneur, maître de toutes choses, je protégerai Zorobabel, fils de Salathiel, Mon serviteur, dit le Seigneur Dieu; et tu seras pour Moi comme un sceau d'alliance, parce que je t'ai choisi, dit le Seigneur tout-puissant.