< Hagai 2 >
1 Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
Le septième mois, le vingt et unième jour du mois, la parole de Yahvé fut adressée à Aggée, le prophète, en ces termes:
2 “Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
Parle à Zorobabel, fils de Shealthiel, gouverneur de Juda, à Josué, fils de Jotsadak, grand prêtre, et au reste du peuple, et dis-leur:
3 ‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
Qui est resté parmi vous, qui a vu cette maison dans sa gloire passée? Comment la voyez-vous maintenant? N'est-elle pas à vos yeux comme un rien?
4 Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Mais maintenant, sois fort, Zorobabel, dit Yahvé. Sois fort, Josué, fils de Jéhozadak, le grand prêtre. Fortifie-toi, vous tous, peuple du pays, dit Yahvé, et travaille, car je suis avec toi, dit Yahvé des armées.
5 ‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
C'est la parole que j'ai promise à vous lorsque vous êtes sortis d'Égypte et que mon Esprit a habité au milieu de vous. N'ayez pas peur.
6 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
Car voici ce que dit l'Éternel des armées: « Encore une fois, c'est encore un peu de temps, et j'ébranlerai les cieux, la terre, la mer et la terre ferme,
7 Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
et j'ébranlerai toutes les nations. Les trésors de toutes les nations viendront, et je remplirai cette maison de gloire, dit Yahvé des armées.
8 ‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
L'argent est à moi, et l'or est à moi, dit l'Éternel des armées.
9 ‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
La dernière gloire de cette maison sera plus grande que la première, dit l'Éternel des armées; et dans ce lieu je donnerai la paix, dit l'Éternel des armées. »
10 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
Le vingt-quatrième jour du neuvième mois, la deuxième année de Darius, la parole de Yahvé fut adressée à Aggée, le prophète, en ces termes:
11 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
« Yahvé des armées dit: Interroge maintenant les prêtres au sujet de la loi, en disant:
12 Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
'Si quelqu'un porte de la viande sainte dans le pli de son vêtement, et qu'avec ce pli il touche du pain, du ragoût, du vin, de l'huile, ou n'importe quel aliment, cela deviendra-t-il saint?'". Les prêtres ont répondu: « Non. »
13 Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
Alors Aggée dit: « Si quelqu'un qui est impur à cause d'un cadavre touche l'un de ces objets, sera-t-il impur? » Les prêtres ont répondu: « Ce sera impur. »
14 Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
Aggée répondit: « Il en est ainsi de ce peuple, il en est ainsi de cette nation devant moi, dit l'Éternel, et il en est ainsi de tout ce que font leurs mains. Ce qu'ils offrent là est impur.
15 “‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
Maintenant, considérez ce qui s'est passé depuis aujourd'hui et en arrière, avant qu'une pierre ne soit posée sur une pierre dans le temple de Yahvé.
16 Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
Pendant tout ce temps, quand on arrivait à un tas de vingt mesures, il n'y en avait que dix. Quand on s'approchait de la cuve à vin pour en tirer cinquante, il n'y en avait que vingt.
17 Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
Je t'ai frappé par le mildiou, la moisissure et la grêle dans tout l'ouvrage de tes mains, et tu ne t'es pas tourné vers moi, dit l'Éternel.
18 ‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
Considérez, je vous prie, depuis ce jour et à rebours, depuis le vingt-quatrième jour du neuvième mois, depuis le jour où les fondements du temple de Yahvé ont été posés, considérez.
19 Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
La semence est-elle encore dans la grange? Oui, la vigne, le figuier, le grenadier et l'olivier n'ont pas produit. A partir d'aujourd'hui, je te bénirai ».
20 Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
La parole de Yahvé fut adressée pour la seconde fois à Aggée, le vingt-quatrième jour du mois, en ces termes:
21 “Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
Parle à Zorobabel, gouverneur de Juda, et dis-lui: « J'ébranlerai les cieux et la terre.
22 Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
Je renverserai le trône des royaumes. Je détruirai la force des royaumes des nations. Je renverserai les chars et ceux qui les montent. Les chevaux et leurs cavaliers tomberont, chacun par l'épée de son frère.
23 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
En ce jour-là, dit Yahvé des armées, je te prendrai, Zorobabel, mon serviteur, fils de Shealtiel, dit Yahvé, et je te rendrai semblable à un sceau, car je t'ai choisi, dit Yahvé des armées. »